Hannes Alfven
From Wikipedia
Hannes Olof Gösta Alfvén (30 Mei, 1908 – 2 Aprili, 1995) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uswidi. Hasa alichunguza uionishaji wa gesi na umuhimu wake kwa chanzo cha ulimwengu. Mwaka wa 1970, pamoja na Louis Neel alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.