Hesabu (Biblia)

From Wikipedia

Kitabu cha Hesabu ni kitabu cha nne katika Agano la Kale au Biblia ya Kiebrania. (Kitabu cha kwanza ni Mwanzo.) Kwa asili kimeandikwa katika lugha ya Kiebrania. Wengine wanakiita Kitabu cha Nne cha Mose (au Musa) kwa vile inafikiriwa kuwa Mose ni mwandishi wa kitabu hicho. Kwa Kilatini kinaitwa Numeri, maana yake “hesabu”. Kinaitwa “Hesabu” kwa vile ndani yake Waisraeli walihesabika mara mbili.

Kitabu cha Hesabu kina sura thelathini na sita, na kinasimulia hasa safari za Waisraeli kutoka Mlima Sinai hadi nchi ya Israeli. Pia, kinataja maagizo mbalimbali ya Mungu na hesabu mbili za Wanaisraeli.