Edward Ngoyai Lowassa

From Wikipedia

Edward Ngoyayi Lowassa (amezaliwa 1953) ni Waziri Mkuu wa kumi wa Tanzania. Amechaguliwa tarehe 30 Desemba, 2005.

Lowassa ni mwenyeji wa Monduli katika Mkoa wa Arusha. Alisoma shahada ya kwanza katika mada ya tamthilia kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, halafu shahada ya pili katika sayansi kwenye Chuo Kikuu cha Bath (Uingereza).

Lowassa ameshika vyeo mbalimbali katika serikali ya Tanzania kama vile:

  • Waziri wa Maji na Mifugo (2000 - 2005)
  • Waziri wa ardhi na makazi (1993 - 1995)
  • Waziri mdogo wa haki na mambo ya bunge katika ofisi ya Makamu wa Rais (1990-1993)
  • Mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (1989 - 1990)
  • Waziri mdogo wa mazingira na mapambano dhii ya umasini katika ofisi ya Makamu wa Rais (1988-2000)
  • Mbunge wa Monduli tangu 1990

[edit] Viungo vya Nje