Genghis Khan

From Wikipedia

Chingis Khan (picha ya karne ya 14 BK)
Chingis Khan (picha ya karne ya 14 BK)
Dola la Chingis-Khan wakati wa kifo chake 1227 BK; mipaka ya nchi za kisasa
Dola la Chingis-Khan wakati wa kifo chake 1227 BK; mipaka ya nchi za kisasa

Genghis Khan (tamka: Chingis Khan, * takriban 1162 – + 18 Agosti, 1227) alizaliwa kama Temujin akawa mfalme mkuu wa Mongolia maarufu katika dunia nzima.

Kwao wengi, Genghis Khan ni sawa na ushindi katili na ya kinyama. Wamongolia siku hizi wanamwona kama Baba yao wa Taifa. Alitumia miaka mingi kuunganisha na kueneza makabila mengi ambayo yalikuwa wakazi wa eneo ambalo sasa linaitwa Mongolia. Baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba alikuwa na kichwa kizuri cha kijeshi kuliko karibu watu wote wengine katika historia ya dunia. Alianzisha ufalme wa Mongolia ambao wengi wanasema ulikuwa eneo kubwa lililounganishwa ambalo halijawahi kupitwa duniani, kutoka mwaka 1206 mpaka kifo chake mwanzoni mwa kipindi cha baridi 1227.

[edit] Viungo vya nje

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Genghis Khan" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Genghis Khan kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.