Ziwa
From Wikipedia
Ziwa ndogo milimani ya Ufaransa
Ziwa ni gimba kubwa la maji linalozungukwa na nchi kavu pande zote. Tofauti na bahari ni ukubwa na kutobadilishana maji na bahari kuu. Lakini maziwa kadhaa yamepewa pia jina la "bahari" hasa kama yana maji ya chumvi au kama watu wa eneo lake hawajui magimba makubwa zaidi ya maji.
Mara nyingi mito inaingia au kutoka katika ziwa.
Maziwa mengi yana maji matamu kama maziwa makubwa ya Afrika ya Mashariki kama vile Viktoria Nyanza au Ziwa Nyasa au maziwa makubwa ya Amerika ya Kaskazini.
Lakini kuna pia maziwa yenye maji ya chumvi kama Bahari ya Chumvi kati ya Yordani na Israel au Bahari ya Kaspi kati ya Urusi na Uajemi.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Ziwa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Ziwa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |
Categories: Mbegu | Ziwa