Berlin

From Wikipedia

Coat of Arms of Berlin
Berlin in Germany

Berlin ni mji mkuu, pia mji mkubwa na jimbo la kujitawala la Ujerumani ikiwa na wakazi 3.8 millioni. Berlin iko mashariki ya Ujerumani, kwa mto unaoitwa Spree.

Berlin ilianza kukua kama mji mkuu wa Prussia. Ilikuwa mji mkuu wa Ujerumani tangu kuundwa kwa Dola la Ujerumani mwaka 1871. Kati ya 1949 na 1991 ilikuwa mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani. Tangu maungano ya Ujerumani ni tena mji mkuu wa Ujerumani wote.

Kati ya 1961 na 1989 mji ilitengwa kwa ukuta kati ya sehemu za mashariki na magharibi.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Berlin" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Berlin kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.