Fasilides wa Ethiopia
From Wikipedia
Fasilides (takriban 1603 – 18 Oktoba, 1667) alikuwa mfalme mkuu wa Uhabeshi kuanzia 1632 hadi kifo chake. Jina lake la kutawala lilikuwa Alam Sagad. Alikuwa ametangazwa kuwa mfalme mkuu mwaka wa 1630 wakati wa uasi wa Sersa Krestos lakini hakuweza kuchukua madaraka mpaka baba yake, Susenyos amejiuzulu. Wakati wa utawala wake Kanisa la kiorthodox lilipata nguvu tena. Fasilides aliwakataa wamisionari Wakatoliki. Pia alikuwa na mabalozi mpaka Uhindi. Aliyemfuata ni Yohannes I.