Kitabu cha Yobu
From Wikipedia
Kitabu cha Yobu ni kitabu katika Agano la Kale, yaani Biblia ya Kiebrania. Pia kinaitwa Ayubu. Kiliandikwa njia ya kishairi, kina sura 42, na swali lake hasa ni “Mbona Mungu aliye mwema anaruhusu mateso?”
Hadithi ya Yobu inasimulia mateso yake Yobu aliyemcha na kumwabudu Mungu vizuri kabisa. Hata hivyo mali yake yote ilipotea, watoto wake wote walikufa, na mke wake alimshauri kumlaani Mungu. Yeye lakini hakufanya kosa mbele ya Mungu. Alipotembelewa na marafiki watatu katika huzuni yake, wanajadiliana sababu ya mateso. Sehemu kubwa ya kitabu inahusu majadiliano hayo. Mwishoni Mungu mwenyewe anamjibu Yobu kutoka katika dhoruba.
Pamoja na vitabu vya Mhubiri na Methali, kitabu cha Yobu ni kitabu kimoja cha fasihi ya hekima ya Biblia.