Melanesia

From Wikipedia

Mahali pa Melanesia katika Pasifiki kaskazini ya Australia
Mahali pa Melanesia katika Pasifiki kaskazini ya Australia
Mwenyeji wa Vanuatu awafundisha watoto kutengeneza moto
Mwenyeji wa Vanuatu awafundisha watoto kutengeneza moto

Melanesia ni eneo la Bahari ya Pasifiki kaskazini ya Australia. Ni moja kati ya makundi makubwa matatu ya visiwa vya Pasifiki pamoja na Mikronesia na Polynesia.

Jina limeundwa na maneno ya Kigiriki ya νῆσος kisiwa na μέλας cheusi yaani "visiwa vyeusi". Mpelelezi na nahodha Mfaransa Jules Dumont d'Urville alitunga jina hili 1832 akitaka kutaja tabia ya wakazi wazalendo waliokuwa na rangi nyeusi-nyeusi.

[edit] Watu na utamaduni

D'Urville alijumlisha wakazi wa visiwa hivi pamoja kutokana na rangi yao. Lakini hali halisi ni watu wa aina mbalimbali. Wengine ni Waaustronesia, wengine Wapapua na wengine watu kutokana na mchanganyiko wa vikundi hivi viwili.

[edit] Nchi za Melanesia

Fiji, Papua Guinea Mpya, Visiwa vya Solomon, Vanuatu na Kaledonia Mpya (chini ya Ufaransa) zinajihesabu kuwa sehemu za Melanesia. Kuhusu visiwa vingine mawazo hutofautiana.

[edit] Visiwa vya Melanesia

Visiwa na funguvisiwa zifuatazo zinahesabiwa katika Melanesia:

Visiwa vilivyoko katika eneo hili lakini wakazi hawajitazami kuwa Wamelanesia:

  • Flores
  • Nauru
  • Sumba
  • Timor

Wakati mwingine hata visiwa upande wa Guinea Mpya vinahesabiwa humo ingawa wakazi hawajitazami hivyo: Halmahera, Alor na Pantar.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Melanesia" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Melanesia kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.