Yerusalemu
From Wikipedia
Yerusalemu | |||
![]() Ukuta wa Maombolezo na Kubba ya Mwamba mjini Yerusalemu |
|||
|
|||
Jina la Kiebrania | יְרוּשָׁלַיִם (Yerushalayim) | ||
Jina la Kiarabu | القـُدْس (al-quds); rasmi: أورشليم القدس (urshalim-al-quds) |
||
Maana ya Jina | Kiebrania: "Urithi wa amani", Kiarabu: "patakatifu" |
||
Utawala | Mji | ||
Wilaya | |||
Wakazi | 724,000 (2006) | ||
Eneo | 126,000 (126 km²) | ||
Meya | Uri Lupolianski | ||
Tovuti rasmi | www.jerusalem.muni.il |
Yerusalemu (Kiebrania ירושלים yerushalayim, kar.: القدس al-quds) ni mji mwenye pande mbili katika Mashariki ya Kati. Kwa upande moja ni mji mkuu wa Israel. Kwa upande mwingine Yerusalemu ya mashariki inatazamiwa kuwa mji mkuu wa Palestina ingawa imetawaliwa na Israel pia tangu 1967. Israel imetangaza tangu 1980 Yerusalemu yote kuwa mji wake mkuu lakini nchi nyingi za dunia hazikubali azimio hili hivyo balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Yerusalemu.
Yerusalemu ina historia ndefu sana. Ni mji muhimu katika dini tatu za Uyahudi, Ukristo na Uislamu.
- Ukuta wa Maombolezo ni patakatifu katika Uyahudi kwa sababu ni mabaki ya pekee ya Hekalu ya Yerusalemu ya zamani za Biblia.
- Kanisa la Kaburi na Ufufuo wa Yesu kama mahali pa ufufuo wake pamoja na mahali pengi panapotajwa katika Agano Jipya ni patakatifu kwa Wakristo.
- Msikiti wa Al-Aqsa pamoja na msikiti wa Kubba ya Mwamba ni mahali patakatifu kwa Waislamu kwa sababu zimetajwa katika Korani; Waislamu huamini ya kwamba hapa ni mahali pa miraji ya Mtume Muhammad.