Stockholm
From Wikipedia
Stockholm ni mji mkuu wa Uswidi pia mji mkubwa wa nchi hii mwenye wakazi 776,000 ambao pamoja na rundiko la mji ni watu milioni 1.2.
Mji uko kwenye pwani la mashariki ya Uswidi ambako ziwa Mälaren lajiunga na Bahari Baltiki. Kitovu cha mji ni visiwa 14 vinavyotengwa na mifereji yenye madaraja.
[edit] Historia
Birger Jarl alianzisha Stockholm mnamo mwaka 1252 BK kama boma la kuzuia maharamia wasiingie kwenye ziwa Mälaren na kushambulia miji huko. Mji ulianza kukua karibu na boma lile ukawa mji wa biashara katika shirikisho la Hanse.
Stockholm ilikuwa mji mkubwa lakini bado mji mkuu kwa sababu wafalme hawakukaa mahali pa kudumu. Gustav Vasa alianzisha makazi ya wafalme mjini.