Msesewe
From Wikipedia
Msesewe ni kiambato cha pombe chenye ungaunga. Unatokana na mti unaoitwa msesewe.
[edit] Utengenezaji
Wapikaji pombe wanabandua magamba ya msesewe, wanaanika kwenye jua, wanayapigapiga mpaka yawe vipande vidogovidogo, ambavyo hupelekwa mashineni kwa kusaga na kuwa katika hali ya unga.
[edit] Utumiaji
Baada ya pombe kupikwa unga wa msesewe huongezwa ili kuongeza ukali wa pombe na pia kuweza kuweka pombe hiyo kukaa kwa muda mrefu. Msesewe hufanya kazi kwa muda wa masaa sita tu pale inapokuwa imepikwa na pombe.