Ladysmith Black Mambazo

From Wikipedia

Ladysmith Black Mambazo ni kundi la muziki ambalo linaimba bila kutumia ala za muziki. Kundi hili lipo Afrika ya Kusini. Neno "Mambazo" linamaanisha "shoka" kwa Kizulu. Na "Ladysmith" ni kitongoji katika jimbo la Natal alichotoka Joseph Shabalala kiongozi na mwanzilishi wa kundi hili.

Ladysmith Black Mambazo lina albamu zaidi ya 40. Kundi hili lilipata umaarufu mkubwa liliposhirikiana na mwanamuziki wa Marekani Paul Simon kutoa albamu ya Graceland ambayo iliwashirikisha pia wanamuziki maarufu duniani kama Miriam Makeba na Hugh Masekela.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Ladysmith Black Mambazo" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Ladysmith Black Mambazo kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.