Minsk
From Wikipedia
Minsk au Miensk (Мінск (Kibelarus) ni mji mkuu na mji mkubwa nchini Belarus. Idadi ya wakazi ni watu milioni 1.8. Mji ulikua kando la mto Svislach.
Jina la mji wa Minsk lilitajwa mara ya kwanza mwaka 1067. Mwaka 1326 ulikuwa sehemu ya dola la Lithuania ukapata cheo cha mji mwaka 1499. Tangu 1793 Minsk ilikuwa sehemu ya Dola la Urusi.
Baada ya mapinduzi ya kikomunisti Minsk ilikuwa mji mkuu wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Kisovyeti ya Belorus ndani ya Umoja wa Kisovyeti.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Minsk" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Minsk kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |