Shubiri

From Wikipedia

Shubiri
Shubiri

Shubiri (pia: shibiri kiar. شبر shibr) ni kipimo cha urefu wa takriban 20 - 25 cm.

Ni kati ya vipimo asilia vya Kiswahili ni umbali mkubwa kati ya kidole gumba na kidole cha mwisho kwenye mkono mmoja.

Inafanana na morta lakini ni ndefu zaidi. Shubiri ni takriban nusu ziraa.

Shubiri si kipimo sanifu lakini katika maisha ya kila siku inasaidia sana. Mtu akijua urefu wa shubiri yake anaweza kupima vitu vingi haraka. Kwa kawaida mtu hutembea na mkono wake kila saa tofauti na futi au chenezo. Hivyo kuna ushauri kila mtu apime shubiri yake na kuikumbuka kwani itamsaidia kila mahali.

[edit] Marejeo

  • makala shubiri katika kamusi ya Velten