Kizu
From Wikipedia
Kuzi | ||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Kizu domo-njano
|
||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||
|
Vizu ni ndege mbua wa jenasi Melierax ya familia Accipitridae. Mgongo na mabawa yao ina rangi ya kijivu na tumbo lao ni mweupe na milia kijivu. Spishi zote zinatokea Afrika kusini kwa jangwa Sahara. Zinapenda mahali pakavu kwenye miti. Hujenga tago lao kwa vijiti juu ya mti na hutaga mayai mawili au matatu, pengine yai moja. Wakati wa majira ya kuzaa huimba kwa milio ya mluzi. Hukamata wanyama na ndege wadogo na wadudu wakubwa.
[edit] Spishi
- Melierax canorus Kizu Kusi (Pale Chanting Goshawk)
- Melierax gabar au Micronisus gabar, Kizu Miguu-myekundu (Gabar Goshawk)
- Melierax metabates, Kizu Domo-jekundu (Dark Chanting Goshawk)
- Melierax poliopterus Kizu Domo-njano (Eastern Chanting Goshawk)