Jean Perrin
From Wikipedia
Jean Baptiste Perrin (30 Septemba, 1870 – 17 Aprili, 1942) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Ufaransa. Hasa alichunguza mada za fizikia ya kiini na kemia ya kifizikia. Mwaka wa 1926 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.