Ukuta wa Maombolezo

From Wikipedia

Mlima wa Hekalu ya Yerusalemu wakati wa Herode
Mlima wa Hekalu ya Yerusalemu wakati wa Herode
Wayahudi wakisali mbele ya Ukuta wa Maombolezo
Wayahudi wakisali mbele ya Ukuta wa Maombolezo
Ukuta wa Maombolezo
Ukuta wa Maombolezo

Ukuta wa Maombolezo (Kiebrania: הכותל המערבי - hakotel hama'ariv "ukuta wa magharibi") katika mji wa kale wa Yerusalemu ni mahali patakatifu wa dini ya Uyahudi.

Contents

[edit] Ukuta wa hekalu ya pili

Ukuta huu ni mabaki yanayoonekana ya hekalu ya Yerusalemu ya pili jinsi ilivyopanushwa na mfalme Herode mnamo 20 KK. Hekalu hii ilibomolewa na Waroma mwaka 70 BK wakati wa vita ya Kiyahudi.

Ukuta si sehemu ya hekalu ile yenyewe bali ilikuwa ukuta wa pembeni wa uwanja uliopo juu ya mlima wa hekalu. Inaaminiwa ya kwamba

[edit] Jina

Jina la "Ukuta wa Maombolezo" limetokana na desturi ya Wayahudi walioonyesha huzuni yao juu ya kuharibiwa kwa hekalu hasa wakisali mahali hapa. Asili ya jina laaminiwa kuwa Kiarabu likaingia katika lugha nyingi. Kwa Kiebrania ukuta huitwa "ukuta wa magharibi" tu na hata jina hili limeenea katika lugha mbalimbali.

[edit] Umuhimu katika imani ya kiyahudi

Wayahudi huheshimu mahali hapa kwa sababu ni sehemu ya hekalu ya Yerusalemu ya mwisho tena sehemu ya mabaki haya yaliyo karibu na mahali pa Patakatifu pa Patakatifu pa hekalu ile.

Wengi huamini ya kwamba Patakatifu pa Patakatifu palikuwa mahali pa kuwepo kwa Mungu duniani ya mlango wa mbinguni ni juu yake. Hivyo ukuta wa magharibi ni sehemu ya karibu na mlango huu. Wayahudi wamehiji kwenda Yerusalemu kwa karne nyingi kwa kusidi ya kusema sala hapahapa.Kuna desturi ya kale ya kuandika maombi kwa karatasi na kuweka karatasi hizi kati ya mawe ya ukuta.

[edit] Fitina juu ya ukuta

Wayahudi walikataliwa kwa muda mrefu kupanda juu ya mlima wa hekalu. Baada ya Yerusalemu kuharibiwa mara ya pili na Waroma mwaka 135 eneo la hekalu pamoja na mji wote likakataliwa kwa Wayudi. Baada ya utekaji wa Kiarabu kulikuwa na vipindi ambako Wayahudi waliruhusiwa kutembelea mlima wa hekalu na vipindi vingine ambako walikataliwa. Hivyo desturi ya kusali mbele ya ukuta wa magharibi ilianza.

Tangu takriban miaka 500 marabbi walianza wengine kufundisha ya kwamba Myahudi asitembee kwenye milima kwa sababu kuna hatari ya kuingia katika sehemu takatifu bila kutakaswa awali; hasa sehemu za patakatifu na patakatifu pa patakatifu ziliruhusiwa kwa makuhani au hata kuhani mkuu pekee. Leo kuna tangazo lenye onyo la Rabbi Mkuu wa Israel mbele ya geti ya kuingia kwenye eneo la mlima wa hekalu linalosema Myahudi asiingie. Ila tu si marabbi wote wanaokubali.

Siku hizi kuna usalama kama kwenye uwanja wa ndege mkali wote wanoelekea ukutani wanapita kwenye geti wanapoangaliwa wakipaswa kufungua mifuko yote. Watu wote wanaruhusiwa kuingia ila tu wanaume wanaombwa kuvaa kofia kufuatana na desturi ya Kiyahudi.