Kiebrania

From Wikipedia

"jisrael" ni neno "Israel" kwa lugha ya Kiebrania na kwa mwandiko wa Kiebrania
"jisrael" ni neno "Israel" kwa lugha ya Kiebrania na kwa mwandiko wa Kiebrania

Lugha ya Kiebrania ni moja ya lugha za kisemiti na lugha ya kitaifa nchini Israel. Ni kati ya lugha za kale duniani. Kiebrania kwa kawaida huandikwa kwa herufi za Kiebrania.

Kiebrania ni lugha ya Torati na maandiko mengine ya Biblia. Sehemu hii ya Kiebrania huitwa "Agano la Kale" katika mapokeo ya kikristo au "tenakh" katika mapokeo ya kiyahudi.

[edit] Lugha ya Kisemiti

Kiebrania pamoja na lugha ya Kiarabu, Kiaramu na Kiamhari (Ethiopia) zinatokana na asili moja ya lugha ya Kisemiti. Kuna lugha nyingi vile vile ambazo zinatokana na asili hii kama Kiashuri na Kifiniki na Kibabili na kadhalika.

[edit] Mwandiko wa Kiebrania

Mwandiko wa lugha hufanywa kwa mwandiko wa pekee unaojulikana tangu miaka 3,000.

Alef Bet/Vet Gimel Dalet He Vav Zayin Khet Tet Yod Kaf/Khaf
א ב ג ד ה ו ז ח ט י כ
ך
Lamed Mem Nun Samekh Ayin Pe/Fe Tsadik Kuf Resh Shin/Sin Tav
ל מ נ ס ע פ צ ק ר ש ת
ם ן ף ץ

[edit] Historia

Kiebrania ilikuwa lugha ya Israeli ya Kale wakati wa Biblia. Baada ya uhamisho wa Babeli Wayahudi walianza kutumia Kiaramu na Kiebrania hakikuzungumzwa tena lakini kilifundishwa kama lugha ya kidini. Wayahudi wa kawaida walitumia katika ibada na wataalamu waliandika vitabu kwa lugha hii.

Katika karne ya 20 Wayahudi wa Ulaya waliamua kukifufusha kama lugha hai. Kimekuwa lugha ya nchi mpya ya Israel tangu 1948. Watu waliohamia Israel kutoka mahali pengi duniani walijifunza Kiebrania na watoto wao wameishika kama lugha yao ya kawaida.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Kiebrania" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Kiebrania kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.