Edith Stein
From Wikipedia
Edith Stein (12 Oktoba, 1891 – 9 au 10 Agosti, 1942) alikuwa mtawa wa kike na mwanafalsafa. Jina lake la utawa lilikuwa Teresa Benedikta wa Msalaba (kwa Kilatini: Teresia Benedicta A Cruce). Aliuawa na wafuasi wa Nazi katika kambi ya wafungwa wa siasa kule Auschwitz. Mwaka wa 1998 alitangazwa kuwa mtakatifu.