Washington
From Wikipedia
Washington ni kati ya majimbo ya kujitawala ya Maungano ya Madola ya Amerika au Marekani. Iko katika kaskazini magharibi ya Marekani bara. Imepakana na Oregon, Idaho na British Columbia katika Kanada. Upande wa magharibi kuna pwani la Pasifiki.
Jina la jimbo lilitolewa kwa heshima ya rais wa kwanza wa Marekani George Washington.
Mji mkuu wa jimbo ni Olympia. Hii ni mji mdogo. Miji miwili mikubwa ya jimbo ni Seattle na Spokane. Eneo la jimbo ni 184,824 km² na idadi ya wakazi inazidi milioni sita.