Waberberi
From Wikipedia
Waberberi ni wakazi asilia wa Afrika ya Kaskazini kuanzia Libya hadi Moroko na nchi za Sahara. Wenyewe wanajiita Amazigh (au: Imazighen) yaani "watu huru".
Leo hii wamepungua kwa sababu wengi wameanza kutumia lugha ya Kiarabu walihesabiwa kati ya Waarabu.
Wanaoendelea kutumia lugha ya Tamazight (au: Kiberber) kama lugha ya kwanza ni takriban theluthi ya watu huko Moroko, asilimia 10-15 nchini Algeria, labda 3 % nchini Lybia. Idadi ndogo zaidi wako Tunisia. Lakhi kadhaa huishi katikam nchi za Sahara kama Mali na Niger halafu kwa idadi ndogo Burkina Faso, Misri na Mauritania. Kutokana na uhamiaji kuna nusi milioni nchini Ufaransa.
Katika nchi kavu jangwani au karibu na jangwa maisha yao ni ya ufugaji na kuhamahama. Mlimani walilima. Leo hii ni hasa Watuareg wanaoendelea na maisha ya kuhamahama.
Katika historia wamejulikana tangu mwanzo wa historia kuandikwa. Waroma na Wagiriki wa Kale waliwaita kwa majina kama Wanumidia, Wagaramanti au Walibya.
Kabla ya unenezaji wa Usilamu wengi walikuwa Wakristo mashuhuri kati hao alikuwa Agostino wa Hippo. Mberberi anayejulikana leo hii ni mchezaji wa mpira Zinédine Zidane.
[edit] Viungo vya Nje
- Richard L. Smith, Ferrum College, What Happened to the Ancient Libyans? Chasing Sources across the Sahara from Herodotus to Ibn Khaldun, Journal of World History, vol. 14, no. 4, 2003 Online article
- Amazigh Startkabel.
- Institut Royal de la Culture Amazighe.
- The New Mass Media and the Shaping of Amazigh Identity.
- Number Systems and Calendars of the Berber Populations of Grand Canary and Tenerife.
- Encyclopedia of the Orient -- Berbers .
- Flags of the World -- Berbers/Imazighen.
- www.mondeberbère.com.
- CMA: Congrès Mondial Amazigh.
- Photo Gallery of Berbers and Touregs from Erg Chebbi area of Moroccan Sahara