Vaal

From Wikipedia

Mto Vaal ni tawimto mrefu wa mto Oranje katika Afrika Kusini. Chanzo chake ni katika milima ya Drakensberg mkoani Mpumalanga mashariki ya mji wa Johannesburg. Inaelekea kusini-magharibi hadi kuungana na mto Oranje karibu na mji wa Kimberley mkoani Northern Cape. Urefu wake ni 1120 km.

Jina la mto limetoka katika lugha ya Kiholanzi; walowezi wa kwanza Waholanzi walitaka kukumbuka mto Waal wa nyumbani kwao.

Vaal ni mto muhimu kwa ajili ya kilimo, viwanda na matumizi ya nyumbani eneo la Johannesburg.

Katika historia ya Afrika Kusini mto Vaal ulikuwa mpaka kati ya koloni ya Uingereza kusini ya mto na jamhuri za makaburu kaskazini ya mto. Jina la kihistoria ya "Transvaal" limemaanisha "ng'ambo ya mto Vaal".