San Jose (Kosta Rika)
From Wikipedia
San José ni mji mkuu wa Kosta Rika. Iko katikati ya nchi kwenye kimo cha 1,170 meters juu ya UB.
Mji ulikuwa na wakazi 309,672 mwaka 2000.
San José ilikuwa kijiji kidogo hadi mwaka 1824. Wakati ule rais wa kwanza wa Kosta Rika huru aliamua kuhamisha mji mkuu kutoka mji wa kikoloni wa Cartago na kuanzisha makao mapya.
1884 San Jose ilikuwa mji wa kwanza wa Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini ya kupata taa za umeme.