Alfabeti

From Wikipedia

Alfabeti ni kiasi cha alama zinazotumiwa kuandika sauti za lugha fulani. Alama hizi hupatikana kama orodha kwa ufuatano uliokubaliwa, kwa mfano "a,b,c,d,e".

Jina la "alfabeti" hutokana na mwandiko wa Kigiriki ambamo herufi mbili za kwanza ni α "alfa" na β "beta".

Alfabeti huonyesha sauti si maneno kamili - hii ni tofauti na mwandiko kama Kichina.

[edit] Mifano ya Alfabeti

Alfabeti inayotumiwa zaidi ni alfabeti ya Kilatini. Lakini kuna alfabeti kadhaa zinazojulikana kimataifa kama vile:

Mengine ni alfabeti kama vile Kikopti, Kigeorgia, Kiarmenia na vingine.

[edit] Abugida

Aina ya pekee za alfabeti ni miandiko ya "abugida". Hii inamaanisha namna ya kuandika ambako hakuna alama za pekee kwa ajili ya vokali. Kila alama ya konsonanti ina namna mbalimbali ya kuonekana kwa kuongeza alama ndogo inayoonyesha ni vokali ipi inayofuata. mifano yake ni

  • alfabeti ya Kiethiopia
  • alfabeti ya Kihindi


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Alfabeti" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Alfabeti kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.