Talk:Tanzania
From Wikipedia
Yah: Orodha ya mikoa. Sijui nani ameweka sanduku lenye majina ya mikoa. Mimi sina uhakika jinsi kuisahihisha. kwa sasa zote ni "Mkow wa..." . Ningeona afadhali kama ni: Arusha, mkoa wa; Mbeya, Mkoa wa... nakadhalika . Je mnaonaje? --Kipala 15:49, 25 Desemba 2005 (UTC)
[edit] Kiswahili
Mwenzetu "196.41.57.3" alibadilisha sentensi juu ya lugha ya Kiswahili. Naona haifai kwa sababu Kiswahili ni lugha ya Kibantu. Na hii imesaidia sana kukubaliwa kwa Kiswhili kwa sababu idadi kubwa ya Watanzania ni wasemaji wa lugha za Kibantu.
Ni kweli ya kwamba Kiswahili kimepokea maneno mengi kutoka lugha nyingi - hasa Kiarabu na Kiingereza - lakini hiyo haibadilihsa tabia yake. Vivyo hivyo Kiingereza ni lugha ya Kigermanik ingawa imepokea takriban 40% ya maneno yake kutoka lugha nyingine hasa Kifaransa ambacho ni lugha ya Kirumi.
Sentensi iliyobadilika inasema sasa ya kwamba Kiswahili ni lugha ya Kiarabu (na kadhalika). Hii si kweli. BAdo ni lugha ya Kibantu. Kwa sababu hiyo nitarudisha lugha ya awali. --Kipala 21:29, 25 Julai 2006 (UTC)