John Bardeen
From Wikipedia
John Bardeen (23 Mei, 1908 – 30 Januari, 1991) alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Marekani. Hasa alichunguza uhandisi wa umeme na kuvumbua transista. Mwaka wa 1956, pamoja na William Shockley na Walter Brattain, na tena mwaka wa 1972, pamoja na Leon Cooper na John Schrieffer alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.