Tumbusi

From Wikipedia

Tumbusi
Tumbusi uso-njano
Tumbusi uso-njano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Falconiformes (Ndege kama kozi)
Familia: Accipitridae (Ndege walio na mnasaba na mwewe)
Jenasi: Aegypius Savigny, 1809

Gypaetus Storr, 1784
Gypohierax Rüppell, 1836
Gyps Savigny, 1809
Necrosyrtes Gloger, 1841
Neophron Savigny, 1809
Sarcogyps Lesson, 1842
Torgos Kaup, 1828
Trigonoceps Lesson, 1842

Tumbusi ni ndege wakubwa wa familia Accipitridae ambao hula mizoga. Wana mnasaba na tai. Huko Marekani kuna ndege wafananao na tumbusi, lakini wale wana mnasaba na makorongo (familia Cathartidae). Tumbusi huvumbua mizoga kwa macho, lakini wale wa Marekani wananusa vizuri pia.

Spishi nyingi za tumbusi zina vichwa bila manyoya. Sifa bainifu hii imekua kuzuia manyoya ya kichwa yasichafuliwe kwa damu wakati tumbusi akiingiza kichwa chake ndani ya mzoga. Kichwa wenye upara kinaweza kusafishwa kwa urahisi ndani ya mto au ziwa.

[edit] Spishi za Afrika

[edit] Spishi za mabara mengine

[edit] Picha