Wilaya ya Pangani

From Wikipedia

Wilaya ya Pangani ni kati ya wilaya za Mkoa wa Tanga katika Tanzania.

Imepakana na wilaya ya Muheza upande wa Kazkazini, Wilaya ya Handeni upande wa magharibi, wilaya ya Bagamoyo (Mkoa wa Pwani) upande wa kusini na Bahari Hindi upande wa mashariki. Makao makuu ya wilaya yako Pangani mjini.


Wilaya ina wakazi 44,107 (2002) [1]. Kuna kata (au shehia, kwa Kiingereza ni Ward) zifuatazo (idadi ya wakazi katika mabano):

Pangani Mashariki (3,079)

Pangani Magharibi (4,949)

Bweni (1,191)

Madanga (3,096)

Kimanga (2,974)

Bushiri (4,348)

Mwera (4,055)

Tungamaa (2,025)

Kipumbwi (4,124)

Mikunguni (3,977)

Ubangaa (2,314)

Mkwaja (3,783)

Mkalamo (4,201)


[edit] Viungo vya Nje

Sensa ya 2002 kwa ajili ya Pangani

Lugha nyingine