Ubuntu

From Wikipedia

Ubuntu ni falsafa ya Kiafrika inayosisitiza mahusiano na ushirikiano wa jamii kama msingi wa maisha bora na amani duniani. Neno ubuntu limetoka kwenye lugha za Kizulu na KiXhosa za Afrika Kusini. Neno la Kiswahili "utu" linabeba, kwa kiasi fulani, maana ya neno ubuntu.

falsafa ya ubuntu imetokana na mila na utamaduni wa Kiafrika ambao umejengwa juu ya maslahi ya jamii zaidi ya maslahi ya mtu binafsi. Msingi wa falsafa hii ni, "mtu sio mtu bila watu," kwa Kizulu, "Umuntu ngumuntu ngabantu." Baadhi ya watu wanaiona falsafa ya ubuntu kuwa na maana nzito ya kiroho na kidini kwakuwa imejengwa juu ya upendo wa watu wengine (kama unavyojipenda wewe) na hata mazingira.

Falsafa hii inaonyesha nafasi ya mtu binafsi katika jamii iliyomzunguka. Ushirikiano ni njia bora ya kuishi kama jamii kuliko ubinafsi.


[edit] Viungo vya Nje