Rhine

From Wikipedia

Rhine (Rhein)
Rhine katika Ujerumani kwenye mwamba wa Loreley
Rhine katika Ujerumani kwenye mwamba wa Loreley
Chanzo Grisons (Uswisi)
Mdomo Bahari ya Kaskazini katika Uholanzi
Nchi Uswisi, Lichtenstein, Austria, Ujerumani, Ufaransa, Uholanzi
Urefu 1,320 km
Kimo cha chanzo 2,344 m
Mkondo 2230 m³/s
Eneo la beseni 185,000 km²

Rhine (tamka: rain) (kwa Kijerumani "Rhein", Kifaransa "Rhin" na Kiholanzi "Rijn") ni kati ya mito mirefu ya Ulaya.

[edit] Chanzo na nchi inapopita

Ramani ya Rhine
Ramani ya Rhine

Ina chanzo chake katika milima ya Uswisi. Inapita katika Uswisi, Ujerumani na Uholanzi; mwendo wake ni pia mpaka kati ya Uswisi na Liechtenstein, Uswisi na Austria halafu Ujerumani na Ufaransa.

Mpakani kati ya Uswisi na Ujerumani mto inapita katika ziwa la Konstanz (au: Bodensee).

[edit] Njia ya maji

Kuanzia mji wa Rheinfelden hadi Rotterdam kwa urefu wa zaidi ya 800 km mto unapitika kwa meli za mtoni.

Usafiri mtoni ni muhimu kwa ajili ya viwanda vingi vilivyopo kando la mto.

Kihistoria Rhine pamoja na mto Danubi ilikuwa mpaka wa kakazini ya Dola la Roma.

[edit] Delta ya Rhine

Ndani ya Uholanzi mto hujigawa kuwa na mikono mikubwa miwili inayoitwa Waal na Lek. Mbele ya mji wa Rotterdam inaungana tena kuwa mto mmoja.


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Rhine" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Rhine kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.