Kijapani
From Wikipedia
Kijapani (日本語 "nihon-go" au "nippon-go" ) ni lugha rasmi nchini Japani. Kinatumiwa na Wajapani karibu wote isipokuwa kundi dogo la Waainu wana lugha yao.
Contents |
[edit] Idadi ya Wasemaji
Kwa jumla kuna wasemaji milioni 124 karibu wote nchini Japan. Kutokana na uhamiaji kuna takriban wasemaji 420,000 katika Marekani (zaidi ya nusu wako Hawaii) na 380,000 huko Brazil.
[edit] Uainishaji
Wataalamu hawakubaliani kuhusu historia ya lugha. Lugha ya karibu ya pekee ni lugha za visiwa vya Ryukyu.
Kijapani inafanana kiasi na Kikorea na kwa kawaida nyingi kimepangwa katika jamii ya lugha za Kialtai. Lakini kuna tabia kadhaa katika Japani ya kale zisizilingana na Kialtai hivyo majadiliano ya kitaalamu yaendelea.
Lugha imepokea maneno mengi kutoka Kichina.
[edit] Mwandiko
Kuna namna tatu ya kuandika:
- hiragana (ひらがな) ni mwandiko wa kawaida. Alama zake zinaonyesha silabi. Watoto wote wanaanza kujifunza kuandika na kusoma kwa hiragana.
- katakana (カタカナ) ni mwandiko wa silabi pia lakini inatumiwa wa njia maalumu. Kama neno linatakiwa kuangaliwa hasa inaoanyeshwa kwa kutumia alama za katakana (kama maandishi manene au ya kiitaliki). Vilevile hutumiwa kwa maneno yasiyo kawaida kama maneno ya kisayansi au maneno ya kigeni.
- kanji (漢字) ni alama za asili ya kichina na kila alama ni neno zima si silabi tu. Kijapanai inatumia alama 2,000 za aina hii.
Inawezekana kuandika Kijapani kwa njia mbili:
a) kama Kiswahili ya kisasa kuanzia upande wa kushoto kwenda kulia
b) Kuanzia juu kwenda chini kwa kutumia nhuzo.
[edit] Mifano
Inayofuata ni mifano ya maneno ya Kijapani:
- 人 (hito) : mtu
- 女 (onna) : mwanamke
- 男 (otoko) : mwanaume
- 水 (mizu) : maji
- こんにちは (konnichiwa) : Habari zako! (wakati wa mchana)
- さよなら (sayonara) : kwa heri
- はい (hai) : ndiyo
- いいえ (iie) : hapana
- スワヒリ語 (Suwahirigo) : Kiswahili
- アフリカ (Afurika) : Afrika
- ケニア (Kenia) : Kenya
- タンザニア (Tanzania) : Tanzania
- ウガンダ (Uganda) : Uganda