Misri ya Kale

From Wikipedia

Piramidi ya Giza pamoja na Sphinx
Piramidi ya Giza pamoja na Sphinx

Misri ya Kale ni ustaarabu uliokuwepo Afrika, sambamba na Naili ya juu, kuanzia kwenye mto wa mkono (ama delta) ya Naili, kaskazini mwa Misri ya Kale kwenda kusini hadi Jebel Barkal, penye maporomoko ya nne, wakati wa kupanuka kwake (Karne ya 15 KK). Ustaarabu huu ulidumu kwa karibu milenia tatu, toka takribani mwaka 3000 KK hadi mwaka 667 BK, na kwisha baada ya Ufalme wa Waaseri kuishinda Misri. Kama ustaarabu uliojishughulisha zaidi na umwagiliaji maji, huu ni mfano mahsusi wa ufalme wa “majimaji”.