Tumbusi
From Wikipedia
Tumbusi | ||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Tumbusi uso-njano
|
||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||
|
Tumbusi ni ndege wakubwa wa familia Accipitridae ambao hula mizoga. Wana mnasaba na tai. Huko Marekani kuna ndege wafananao na tumbusi, lakini wale wana mnasaba na makorongo (familia Cathartidae). Tumbusi huvumbua mizoga kwa macho, lakini wale wa Marekani wananusa vizuri pia.
Spishi nyingi za tumbusi zina vichwa bila manyoya. Sifa bainifu hii imekua kuzuia manyoya ya kichwa yasichafuliwe kwa damu wakati tumbusi akiingiza kichwa chake ndani ya mzoga. Kichwa wenye upara kinaweza kusafishwa kwa urahisi ndani ya mto au ziwa.
[edit] Spishi za Afrika
- Aegypius monachus, Tumbusi Mweusi (Eurasian Black Vulture or Monk Vulture)
- Gypaetus barbatus, Tumbusi Mlakondoo (Lammergeier or Bearded Vulture)
- Gypohierax angolensis, Tumbusi Miwese (Palm-nut Vulture)
- Gyps africanus, Tumbusi Mgongo-mweupe (White-backed Vulture)
- Gyps coprotheres, Tumbusi Kusi (w:Cape Vulture:Cape Vulture)
- Gyps fulvus, Tumbusi wa Ulaya (Eurasian Griffon Vulture)
- Gyps rueppellii, Tumbusi Mbuga (Rüppell's Griffon Vulture)
- Necrosyrtes monachus, Tumbusi Kapuchini (Hooded Vulture)
- Neophron percnopterus, Tumbusi Uso-njano (Egyptian Vulture)
- Torgos tracheliotus, Tumbusi Ngusha (Nubian or Lappet-faced Vulture)
- Trigonoceps occipitalis, Tumbusi Kichwa-cheupe (White-headed Vulture)
[edit] Spishi za mabara mengine
- Gyps bengalensis (Indian White-rumped Vulture)
- Gyps indicus (Long-billed Vulture)
- Gyps himalayensis (Himalayan Griffon Vulture)
- Sarcogyps calvus (Red-headed Vulture)