Ganda la dunia
From Wikipedia
Ganda la dunia ni tabaka ya juu ya sayari yetu. Ni sehemu ya tabakamwamba.
Ganda ni jumla la mabamba yanayosukumwa na nguvu ya shindikizo kutoka kitovu cha dunia.
Mwamba wa ganda hutokea pale ambako magma (yaani mwamba moto wa kiowevu) inapanda juu kwenye migongo iliyoko katikati ya msingi wa bahari inapopoa na kuganda.
Kinyume chake sehemu za ganda la dunia huzama chini pale ambako bamba moja linajisukuma chini ya bamba lingine na kuyeyuka katika magma ya koti ya dunia.
Categories: Jiolojia | Gandunia | Sayansi za dunia | Jaribio | Mbegu