Bustani ya wanyama
From Wikipedia

Kitengo cha Panda kwenye bustani ya wanyama ya Chiang Mai (Uthai)

Wageni wanalisha na kushika panyabuku waliozoea binadamu kwenye bustani ya wanyama ya Parc Animalier des Pyrenées, Ufaransa
Bustani ya wanyama ni mahali ambapo wanyama hasa wanyamapori wa aina mbalimbali wanatunzwa ili watu wapate kuwatazama.
Siku hizi bustani ya wanyama zimekuwa pia mahali pa kutunza spishi au aina za wanyama walioko hatarini ya kwisha.
Miji mingi mikubwa duniani ina bustani ya wanyama. Watu hulipa kiingilio wakitaka kuingia. Lakini hata hivyo bustani hizi hazipokei mapato ya kutosha hivyo hazina budi kupokea pia misaada kutoka serikali.
Umuhimu wa bustani za wanyama ni katika
- kuwapatia watu nafasi ya kuona kwa macho yao wanyama wa nchi zilizo mbali
- kuwaelimisha watu juu ya wanyama wa dunia pia kuhusu mazingira yao
- kuwa kituo cha utafiti wa kisayansi kuhusu wanyama
- kuhifadhi na kufuga aina za wanyama hatarini ya kwisha hasa wasio na mazingira asilia tena