Kelvini

From Wikipedia

Kelvini ni kipimo cha SI kwa halijoto. Alama yake ni K.

Kiwango chake kinaanza kwenye sifuri halisi (= -273.15 °C) pasipo na mwendo wowote wa molekuli. Kizio kimoja cha Kelvini ni sehemu ya 1/273.16 ya tofauti kati ya sifuri halisi (=0 K) na kiwango utatu cha maji (+0.01 °C).

Skeli ya Kelvini ililinganishwa na skeli ya selsiasi yaani kizio kimoja cha Kelvini ni sawa na kizio kimoja cha Selsiasi. Skeli ya Kelvini haihitaji namba za minusi (-) kwa sababu hakuna hali chini ya 0 K.

Jina limetokana na mwanafisikia Mwingereza William Thomson aliyekuwa na cheo cha Lord Kelvin (1824–1907).