Luxemburg (mji)
From Wikipedia
Luxemburg (Kiluxemburg: Lëtzebuerg, Kifaransa:Luxembourg; Kijerumani: Luxemburg) ni mji mkuu wa Utemi wa Luxemburg katika Ulaya ya Kati.
Mji ulikuwa na wakazi 76,420 mnamo mwaka 2005. Iko katika kusini ya nchi ambako mito ya Alzette na Pétrusse inaungana.
Mji wa Luxemburg ni kati ya miji tajiri za Ulaya. Uchumi umekua sana upande wa benki na biashara. Luxemburg ni pia moja kati ya miji mikuu ya Umoja wa Ulaya pamoja na Brussels na Strasburg. Mahakama Kuu ya Ulaya ina makao makuu hapa pia Mamlaka Kuu ya Ukaguzi wa Ulaya na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya.
Mji wa Kale ya Luxemburg iliingizwa na UNESCO katika orodha la urithi wa dunia.