Korongo (Gruidae)

From Wikipedia

Korongo
Korongo-taji
Korongo-taji
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Gruiformes (Ndege kama makorongo)
Familia: Gruidae (Ndege walio na mnasaba na makorongo)
Vigors, 1825
Jenasi: Angalia katiba

Makorongo hawa ni ndege wa familia Gruidae wenye domo fupi na jembamba kuliko lile la makorongo wa familia Ciconiidae. Spishi nyingi hufanya mikogo ya kubembeleza jike wakitoa sauti kubwa. Huugana kwa maishi yao yote. Spishi za nchi za halijoto wastani huhama kila mwaka kabla ya wakati wa baridi. Makorongo hawa hupenda kuwa pamoja na huhama kwa makundi makubwa. Hula kila kitu kinachopatikana, kama panya, watambaazi, amfibia au samaki, hata nafaka na matunda madogo. Spishi za makorongo zinatokea mabara yote ghairi ya Marekani ya Kusini.

[edit] Spishi za Afrika

[edit] Spishi za mabara mengine

[edit] Picha