IMF
From Wikipedia

Jengo la makao makuu ya IMF mjini Washington DC
IMF (International Monetary Fund) ni Shirika la Fedha la Kimataifa. Lilianzishwa mwaka 1946 kwa shabaha ya kuboresha ushirikiano katika mambo ya fedha duniani. Kuna nchi wanachama 184. Makao makuu yapo Washington DC nchini Marekani.
Kazi yake ni kuangalia siasa ya fedha na benki duniani na kuifanyia utafiti. Inatoa misaada na ushauri ikitakiwa.
Si shirika halisi la Umoja wa Mataifa lakini hushirikiana na UM. Nchi tajiri za Ulaya pamoja na Marekani zinaongoza IMF kwa sababu ni nchi zilizoweka pesa zaidi katika mfuko wake. Mwenyekiti wa IMF huwa anatoka katika nchi za Ulaya na makamu wake ni kutoka Marekani.
IMF hushirikiana karibu na Benki ya Dunia.
[edit] Viungo vya Nje
![]() |
Makala hiyo kuhusu "IMF" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu IMF kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |