Talk:Yohane IV

From Wikipedia

Samahani, Kipala, lakini kulikuwa na makala kuhusu Yohannes IV wa Ethiopia ila haikuwa na habari zaidi kuliko ya kwako. Naomba uangalie Watawala wa Uhabeshi kwa jinsi nilivyoandika majina ya akina Negus. Asante. --Oliver Stegen 20:36, 20 Septemba 2006 (UTC)

Uliweka kiungo - asante. Kuhusu tahijia ya majina tuna eneo pana sana. Sijui... Mimi ningependelea kufuata tahijia ya Biblia ya Kiswahili (ila tu: Union au Kisasa??) kama ni jina la Kibiblia. Isipokuwa kwa majina ya Kiingereza n.k. Sina uhakika kama itafaa. Tuone. Sawa? --Kipala 20:49, 20 Septemba 2006 (UTC)
Hamna shida. Nilianza kutumia jina lilivyotumika kwenye wikipedia nyingine kwa vile ilionekana kama walinukuu herufi za Kiamhara kwa mfumo wa Kilatini (transliteration?). Ndiyo sababu nilianza na maorodha (angalia pia Wafalme Wakuu wa Japani). Angalao tungeweza kubofya kiungo kwenye orodha. Kwa leo nasema 'Usiku mwema'. --Oliver Stegen 21:00, 20 Septemba 2006 (UTC)