Moshi (mji)
From Wikipedia

Moshi ni makao makuu ya mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania. Kabila linalopatikana katika mji huu ni la Wachagga. Wachagga wanapenda vyakula vinavyopikwa kwa kutumia ndizi kama vile mtori, kitawa, na [[machalari. Wakazi wengi wa moshi ni wakulima, wafugaji na wafanyabiashara. Mji wa Moshi una mandhari nzuri ya kuvutia watalii.
Mji wa Moshi una vyuo vikuu vitatu: MUCCoBS ( Moshi University College Of Cooperatives and Business Studies) ambacho ni chuo kikuu kishiriki cha Sokoine University of Agriculture (SUA)Morogoro MWUCE ( Mwenge University College Of Education ) ambacho ni chuo kikuu kishiriki cha SAUT ( St. Augustine University-Mwanza KCMC Medical School chini ya chuo kikuu cha Tumaini-Iringa
Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002, mji huu una wakazi wapatao 144,739. Kabila linaloongoza kwa idadi ya wakazi wa mji wa Moshi ni Wachagga. Kuna makabila mengi kama Wapare, Wanyakyusa,Wasukuma, Warangi,Wasambaa n.k.
Moshi ni mji wenye baridi katika miezi ya Juni mpaka Agosti na kipindi cha joto katika miezi ya Oktoba hadi katikati ya Januari.
Watu wengi wanaenda Moshi kufanya kazi na kurudi nyumbani jioni. mji wa moshi idadi kubwa ya wakazi wake ni wachaga.watalii hupenda sana mji wa moshi kwa sababu ya mlima kilimanjaro na huduma muhimu kama mahoteli na usafiri.