Ugiriki ya Kale

From Wikipedia

Ugiriki ya Kale ni kipindi katika historia ambapo Ugiriki ilipanuka katika eneo kubwa la Mediteraneo na Bahari Nyeusi, na kudumu wa karibu milenia moja, hadi Ukristo ulipoanza. Unadhaniwa na wanahistoria wengi kuwa ni utamaduni anzilishi wa Ustaarabu wa Magharibi. Utamaduni wa Kigiriki ulikuwa na nguvu kubwa ya ushawishi katika Ufalme wa Rumi, ambao ulibeba sehemu ya utamaduni huo katika sehemu nyingi za Ulaya.

Ustaarabu wa Ukiriki ya kale umeathiri pia lugha, siasa, mifumo ya elimu, falsafa, sayansi, sanaa, ufundi sanifu wa dunia ya sasa, na kuchochea Mwamko Mpya katika Ulaya Magharibi; na kuchipuka tena katika vipindi mbalimbali vya uamsho wa tamaduni za kisasa za Kigiriki, ndani ya karne ya 18 na 19 katika Ulaya na Amerika.