Zauditu wa Uhabeshi
From Wikipedia
Zauditu (29 Aprili, 1876 – 2 Aprili, 1930) alikuwa malkia mtawala wa Uhabeshi kuanzia 27 Septemba 1916 hadi kifo chake. Alimfuata Iyasu V. Jina lake la kubatizwa lilikuwa Askala Maryam. Alikuwa mtoto wa kwanza wa Menelik II. Mwanzoni utawala wake ulisumbuliwa na uasi wa Iyasu aliyekuwa ameuzuliwa. Malkia huyu anajulikana kwa jinsi alivyopenda dini na alivyokuwa mpinzani mkubwa wa mabadiliko aliyokuwa akiyafanya Ras Tafari Makonnen. Zauditu aligombana sana naye Makonnen, kuhusu mambo ya siasa lakini alishindwa. Naye Tafari alimfuata kama mfalme chini ya jina la Haile Selassie.