John F. Kennedy
From Wikipedia
John Fitzgerald Kennedy (29 Mei, 1917 – 22 Novemba, 1963) alikuwa Raisi wa Marekani. Alikuwa mtoto wa pili katika familia ya watoto 9. Baba yake alikuwa mfanyabiashara maarufu. Ukoo wa kenedi una asili ya irish, vita kuu ya pili ilipoanza alijiunga na jeshi la wanamaji. 1943 alijeruhiwa katika shambulio lilifavywa na ndege za kivita za japani. Mwaka 1947 alianza kujiingiza katika siasa na 1960 alichaguliwa kuwa Rais wa Amerika. Aliuwa kwa kupigwa risasi tarehe 22 Novemba, 1963. Atakumbukwa pia kwa kutetea haki za watu wote bila kujali rangi.
Alisema "Wamarekani wasiulize Marekani imewatendea nini bali wajiulize kwanza wao wenyewe wameitendea nini nchi yao".