Nigeria

From Wikipedia

Federal Republic of Nigeria
Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria
Flag of Nigeria Nembo ya Nigeria
Bendera Nembo
Wito la taifa: Unity and Faith, Peace and Progress (Umoja na Imani, Amani na Maendeleo)
Wimbo wa taifa: Arise O Compatriots, Nigeria's Call Obey (Amkeni wananchi, mtieni wito la Nigeria)
Lokeshen ya Nigeria
Mji mkuu Abuja
9°10′ N 7°10′ E
Mji mkubwa nchini Lagos
Lugha rasmi Kiingereza
Serikali
Rais
Shirikisho la Jamhuri
Olusẹgun Ọbasanjọ
Uhuru
kutoka Uingereza
Oktoba 1 1960
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
923,768 km² (ya 31)
1.4%
Idadi ya watu
 - 2005 kadirio
 - 1991 sensa
 - Msongamano wa watu
 
131,530,000 (ya 9)
88,992,220
142/km² (ya 53)
Fedha Naira (₦) (NGN)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+1)
(UTC+2)
Intaneti TLD .ng
Kodi ya simu +234

Nigeria (kisw. pia: Nijeria au Naijeria) ni nchi ya Afrika ya Magharibi kwenye pwani la Bahari Atlantiki. Imepakana na Benin, Niger, Chad na Kamerun. Mji mkuu tangu ni Abuja ikitanguliwa na Lagos hadi mwaka 1991. Nigeria imepata uhuru wake mwaka 1960 ni nchi ya Afrika yote yenye watu wengi.

Contents

[edit] Jiografia

Nigeria inaunganisha maeneo tofauti sana ikiwa na msitu wa mvua katika kusini kupitia nchi ya savana hadi kanda ya Sahel na mwanzo wa jangwa la Sahara kaskazini kabisa. Mlima wa juu ni Chappal Waddi yenye 2,419 m juu ya UB.

Hali ya hewa ni ya kitropiki. Kusini kuna mvua mwaka wote lakini kaskazini ya nchi kuna ukame kati ya Novemba na Aprili.

Mito mikubwa ni mto Niger na mto Benue; yote miwili inakutana na kuishia katika delta ya Niger ambayo ni kati ya delta kubwa zaidi duniani.

Mji mkubwa ni Lagos (mji mkuu wa zamani); kati ya miji mingini ni Abuja, Kano, Ibadan, Oshogbo, Ilorin, Abeokuta, Ogbomosho na Port Harcourt.

Nigeria - Madola ya shirikisho na nchi jirani
Nigeria - Madola ya shirikisho na nchi jirani

[edit] Madola ya shirikisho

Muundo wa Nigeria ni Shirikisho la Jamhuri. Katiba ya nchi imefuata mfano wa katiba ya Marekani. Rais huchaguliwa na wananchi wote ndiye mkuu wa serikali. Anawajibika mbele ya bunge yenye vitengo viwili: Senati na Baraza la Wawakilishi.

  • Abia
  • Adamawa
  • Akwa Ibom
  • Anambra
  • Bauchi
  • Bayelsa
  • Benue
  • Borno
  • Cross River
  • Delta
  • Ebonyi
  • Edo
  • Ekiti
  • Enugu
  • Federal Capital Territory
  • Gombe
  • Imo
  • Jigawa
  • Kaduna
  • Kano
  • Katsina
  • Kebbi
  • Kogi
  • Kwara
  • Lagos
  • Nassarawa
  • Niger
  • Ogun
  • Ondo
  • Osun
  • Oyo
  • Plateau
  • Rivers
  • Sokoto
  • Taraba
  • Yobe
  • Zamfara
Kisiwa cha Lagos, mbele wangwa
Kisiwa cha Lagos, mbele wangwa

[edit] Wakazi

Nigeria hukadiriwa kuwa na wakazi takriban milioni 130. Vikundi vikubwa katika jumla la makabila 300 ni Wahaussa na Wafulani katika kaskazini (jumla 20-30%), Waigbo (Waibo) katika kusini (14-18%), Wayoruba katika sehemu za magharibi (20-27%). Makadirio ya idadi yanatofautiana sana ni vigumu kupata namba halisi kwa sababu ya umuhimu wake wa kisiasa.

[edit] Dini

Kuthebitisha idadi ya wafuasi wa dini mbalimbali ni vigumu vilevile. Kwa ujumla kaskazini ya nchi ina historia ndefu ya Uislamu na wakazi ni Waislamu hasa Wahaussa. Kusini kuna Wakristo wengi, Waigbo ni zaidi Wakatoliki na Yoruba zaidi Waprotestant. Wengine wanasema ya kwamba idadi za Wakristo na za Waislamu zinalingana - wengine wanaona Waislamu ni wengi kidogo labda 50%, Wakristo 40% na wafuasi wa dini za jadi takriban 10%.

Olusegun Obasanjo Rais wa Nigeria 1999 - 2007
Olusegun Obasanjo Rais wa Nigeria 1999 - 2007

[edit] Historia

Kabla ya ukoloni eneo la Nigeria ilikuwa na falme mbalimbali. Kaskazini ilikuwa chini ya sultani za Kiislamu za Kano na Sokoto; kusini ilikuwa na falme za Benin, Ife na Oyo. Kwa jumla eneo la Nigeria haikuwahi kuwa pamoja kabla ya kuja kwa wakoloni waliochora mipaka yao bila kujali mno tamaduni za wenyeji. Ilikuwa azimio la Uingereza kuunganisha maeneo yenye utamaduni na historia tofauti kuwa koloni moja.

Nigeria ilipata uhuru wake tarehe 1 Oktoba 1960 kutoka kwa Uingereza.

Kati ya 1967-1970 nchi iliona vita ya wenyewe kwa wenyewe; magharibi ya nchi inayokaliwa na Waigbo hasa ilijaribu kujitenga wa jina la Biafra wakipinga utawala wa wanajeshi Waislamu. Takriban watu milioni 2 walikufa na njaa wakati ule.

Nigeria iliendelea kuvurugika na mapinduzi ya kijeshi. Tangu miaka ya 1970 Nigeria ilikuwa na mapato makubwa kutokana na mafuta yaliyotolewa kutoka ardhi yakwe hasa katika delta ya mto Niger. Ulaji rushwa na ufisadi wa watawala wa kijeshi ulizuia maendeleo ya nchi jinsi ilivyoonekana katika nchi nyingine yenye mafuta.

Tangu 1999 nchi ilirudi kwa utawala wa kisheria ikapata katiba mpya na kumchagua rais Olusegun Obasanjo aliyerudishwa madarakani mara moja. Majaribio ya wafuasi wake wa kubadilisha katiba na kumpa kipindi cha tatu yameshindikana bungeni. Rais mpya atakeyemfuata Obasanjo atachaguliwa katika kura ya mwaka 2007.




Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia
Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Nigeria" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Nigeria kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.