Siku

From Wikipedia

Siku ni muda wa wakati wa masaa 24 ambamo tunaona vipindi viwili vya mwanga wa mchana na giza ya usiku.

[edit] Mchana na usiku

Mabadiliko haya ya mchana na usiku husabibishwa na mzunguko wa dunia kwenye kipenyo chake. Upande wa dunia unaotazama jua unaona mwanga wa mchana; dunia ikizunguka kwenye kipenyo chake mahali petu tunapokaa panafika upande mwingine ulio mbali na jua sasa tunaangalia giza ya angani na kuona usiku.

[edit] Muda wa siku

Mzunguko huo una muda wa nukta (sekondi) 86,400 au masaa 24.

Kwa sababu muda wa mzunguko haulingani kamili na kipimo cha sekondi kuna siku ndefu au fupi zinazopatikana kwa kuingiza au kupunguza nukta moja kufuatana na azimio ya wataalamu wa wakati. Hii haina umhimu wowote katika maisha ya kila siku lakini inapaswa kuangaliwa pale ambako saa kamili sana ya kiatomi hutumiwa.