Mogadishu
From Wikipedia
Mogadishu (maandishi wa Kisomali Muqdisho, wa Kiitalia Mogadiscio) ni mji mkuu wa Somalia. Iko ufukoni wa Bahari Hindi ikiwa na wakazi kati ya milioni 1.5 na 3. Idadi kamili haijulikani kutokana na hali ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ya miaka iliyopita.
Mohadishu imeundwa mnamo mwaka 900 BK ikawa mji wa kaskazini kabisa wa utamaduni wa Waswahili kwenye pwani la Afrika ya Mashariki. Ilikuwa sehemu ya biashara ya kimataifa ya Waswahili jinsi inavyonekana kutokana na sarafu za kale za Uchina, Sri Lanka na Vietnam zilizokutwa na wanaarkiolojia katika ardhi yake.
Msafiri Mwarabu Ibn Battuta alitembelea Mogadishu mnamo mwaka 1300 akaona matajiri akataja "watu wanene wengi". Mji ulikuwa na vipindi vya kujitegemea na vipindi vya kutawaliwa na nchi za nje katika historia yake. Mnamo mwaka 1500 Wareno walikuwa mabwana wake. Tangu katikati ya karne ya 19 BK Mogadishu ilikuwa chini ya sultani wa Zanzibar.
1892 sultani alikodisha mji kwa Italia iliyoinunua 1905 kutoka kwake ukawa mji mkuu wa koloni ya Somalia ya Kiitalia. Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mji ulivamiwa na Waingereza mwaka 1941 waliourudisha kwa Itala 1954.
Tangu uhuru 1960 Mogadishu ikawa mji mkuu wa Somalia.
1990 dikteta Siad Barre alipinduliwa halafu Mogadishu pamoja na nchi yote iliingia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe. Wanajeshi wa Marekani walijaribu mwaka 1993 kurudisha hali ya usalama kwa niaba ya Umoja wa Mataifa lakini walikuta upinzani mkali kutoka kwa vikundi vya wanamgambo Wasomalia. Baada ya kupoteza askari Marekani iliondoka tena.
Hali ya vita imeendelea.