Tido Mhando

From Wikipedia

Tido Mhando ni mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC.

Tido Mhando ni mmoja wa watangazaji mahiri na wakongwe Tanzania imewahi kuwa nao.Alianzia redio ya taifa, Radio Tanzania Dar Es Salaam, kabla ya kuelekea Kenya ambako alifanya kazi kwa miaka mingi kabla ya kujiunga na shirika la utangazaji la Uingereza, BBC.

Baada ya kuhamishia makazi yake London, Tido Mhando alipewa majukumu ya ukuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC mwaka 1999.Katika muda wake madarakani, Idhaa ya Kiswahili imepata mafanikio makubwa, ikiwa ni pamoja na idadi ya wasikilizaji kupanda mpaka milioni 19.

Anatarajiwa kustaafu mwishoni mwa mwezi Oktoba, akitarajia kurejea nyumbani Tanzania ambako haijajulikana atapewa majukumu gani.


[edit] Viungo vya nje