User talk:Ndesanjo
From Wikipedia
Contents |
[edit] Welcome!
Habari, Ndesanjo. We are working on improving the site (you too, I think!). Don't forget to visit Wikipedia:Jumuia, and check out Recentchanges from time to time. Don't hesitate to correct bad Swahili you find here. Sj 01:53, 24 Septemba 2005 (UTC)
[edit] Jina la makala
Habari Ndesanjo? Nataka kukujulisha kwamba ukiandika makala, uhakikishe jina lake likitamkwa mara ya kwanza (kwa kawaida mwanzoni kabisa) liwe nene kama hili. Kwa mfano, angalia nilivyobadilisha makala Ellen Johnson-Sirleaf. Ili neno liwe nene, una weka ''' kabla na baada yake. Ahsante sana. Marcos 11:42, 21 Novemba 2005 (UTC)
Marcos, asante kwa kunijulisha. Hongera kwa kazi ufanyanyo!
[edit] Naomba angalia utoe shauri
Ndesanjo: nimeweka swali kwa ukurasa wa Marcos [[1]] akiwa mratibu - wewe ukiwa Mswahili kabisa uangalie utoe shauri. Naomba sana. Ukiona vema labda kuna wataalamu ambao wangejua jibu tukibaki na wasiwasi kati yetu. --Kipala 21:03, 17 Januari 2006 (UTC)
[edit] Swahili help
Hi, I have a Swahili question for you. w:Span (unit) lists a Swahili term "unguru" as a unit of measurement. I believe this is a hoax, based on this Slashdot post. Also: w:Fungu'lu. Could you help? Cheers and thanks, w:User:AxelBoldt
Hi Boldt, I've never heard the two terms before. I am not sure if they are swahili terms. I will ask some people around the swahili term for that unit of measurement.
- Hi, I just did a search of my own after noticing this, and looks like the correct Swahili word for that unit of measurement is futuri. I just now added that correct word to the English article too. 70.105.38.244 22:58, 17 Desemba 2005 (UTC)
Thanks a lot. Now I know what "futuri" means.
- Hi, my "Kamusi ya Kiswahili Sanifu" says: futuri is another word for shubiri which means urefu kutoka kidole gumba hadi cha kati (=a "span", isn´t it? from thumb to middle finger) kiasi cha inchi tisa (=9"); same as "shibiri". But then I am not sure if to absolutely trust the Kamusi in this detail because my two other dics say:
Madan-Johnson: futuri,a short span, as a measure, from the tip of the thumb to the tip of the forefinger; as distinct from shibiri, a full span from thumb to little finger; > arab. ftr / shbr
Velten (1910) has the same as Madan-Johnson on futuri and on shibiri / shubiri;
so even if the two are Wazungu my guess would be that they noted a difference of measures well aware among the Waswahili themselves which may have been lost later - and that the recent kamusi either reflects that the two are mixed up or they had the wrong reference people. --Kipala 19:15, 5 Januari 2006 (UTC)
-
- I have also checked my Arabic dics; one says shibr ﺷﺒﺮ is the span of the hand and futra ﻓﺘﺮﻩ is the span of time; the other one gives futr ﻓﺘﺮ as the span between extended thumb and index finger.I guess as both Swahili words are of Arab origin then older dics are probably right. --Kipala 20:23, 5 Januari 2006 (UTC)
[edit] alf lela
Ndesanjo, hujambo? Hongera na makala mapya ya alf lela.. Nimeongeza maneno mawili kuhusu Baghdadi - wakati wa kukusanyika kwa hadithi hizi ilikuwa makao makuu ya Khalifa na hivyo kituvo cha Uislamu duniani. --Kipala 22:06, 17 Desemba 2005 (UTC)
Kipala, asante sana. Hongera kwa kazi zako. Tuendelee hivi hivi iko siku watakuja wengi zaidi kusaidia. Safi kwa nyongeza yako kwenye Alfu Lela U Lela. Bado nitaipitia tena kuiboresha.
[edit] Abu Nuwas
Ndesanjo, hujambo? Umefika vizuri mwaka mpya? Safari hii naona tatizo na mabadiliko yako Abu Nuwas > Abunuwasi.
Kwa sababu mbili: kwanza nimeshaweka viungo mbalimbali vya Abu Nuwas.
Pili - hapa tunahitaja maelewano kati ya watu wanaochangia kuhusu maswali jinsi ya kutaja vitu. Jina la mtu huyu mshairi mwarabu ni Abu Nuwas - Abunuwasi inaweza kuchukuliwa kwa namna mbili: AMA (ninavyoona) ndiye huyu jamaa wa kifasihi wa "Riwaya" aliye tofauti na Abu Nuwas wa Kihistoria AU ni jina la Kiswahili kwa ajili ya mshairi mwarabu Abu Nuwas; lakini hata kama mimi si mtaalamu katika mambo haya sidhani ni hivyo.
Unaonaje? Sipendi kabisa tupate hivi "vita vya wahariri" jinsi ilivyo katika wikipedia nyingine --Kipala 19:15, 5 Januari 2006 (UTC)
-
- Mimi sijui sana Unguja lakini hata huko naona watu wanaweza kutumia ile "Abu" kuwa sehemu ya jina lao wakiiandika pekee; kwa mfano Sheikh Sayyid bin Omar bin Abdullah bin Abu Bakr bin Salim (1917-1988) aliyekuwa mkuu wa Chuo cha Kiislamu Zanzibar; ninavyoona jina la "Abu Bakr" hutumiwa na Waswahili Waislamu wengi bila kuibadilisha kuwa "Abubakri" au "Abubekri". Unaonaje, si kweli?? --Kipala 19:33, 5 Januari 2006 (UTC)
Ndio Kipala. Asante, mwaka mpya salama kabisa. Hongera sana kwa kazi zako. Umeichangamsha kamusi elezo yetu. Sasa kwenye Abu Nuwas/Abunuwasi. Ni kweli hakuna haja ya kuingia kwenye vita wanavyofanya wengine. Nakubaliana nawe kuhusu jina lake halisi. Nadhani kuna majina ambayo yanapoingia kwenye Kiswahili yanabadilika kama vile Yesu. Jina lake hasa la kule alikotokea halitumiki. Au nabii Musa. Lakini kuna mengine yanabaki vile vile. Sasa katika vitabu kadhaa vya Kiswahili ambavyo nimewahi kuvipitia, nimeona jina lake limechukua kanuni fulani za Kiswahili (kwa mfano badala ya kuishia na "s" pekee ikaongezwa "i" kuwa Abunuwasi). Lakini hii inafanya jina hilo kuwa moja wakati ambapo katika maelezo yako ni kuwa haya ni majina mawili (sio?). Sasa tunaweza kuchukua vile Waswahili walivyotamka na kuandika jina lake au tukachukua jina lake halisi, ambapo itakuwa ni majina mawili kama ulivyoandika. Tunachoweza kufanya naona ni kuandika jina lake hasa (yaani lake na la ubini) kisha tukaeleza kuwa Waswahili wamekuwa wakimwita Abunuwasi. Unasemaje?
- Asante kwa jibu la haraka. Kimsingi mimi naona Abunuwasi (jamaa wa kifasihi) wa "Riwaya" na mshairi Abu Nuwas (mtu wa kihistoria) si yeye yule.
Abu Nuwas alitoa jina lake kwa Abunuwasi (au labda zaidi: jina lake limechukuliwa) - hadithi zile za Abunuwasi zimesimuliwa kati ya Waturuki juu ya Nasreddin na kati ya Waarabu wengine juu ya Guha (ninaandaa makala nyingine kuhusu Riwaya nitakapoeleza uhusiano huo).
Lakini hadithi za Riwaya hazina uhusiano na Abu Nuwas wa kihistoria. Hapo sababu yangu ya kuwataja pekee.
>> Ninahamisha majidiliano yetu kwenye ukurasa ya Abu Nuwas - sawa? ----Kipala 13:07, 6 Januari 2006 (UTC)
Kipala, nimekupata sawasawa sasa. Nashukuru. Nilichanganya mambo. Nakupa pongezi tena kwa kazi zako. Tuendelee.
[edit] Maajabu ya Kwanzaa
Ndesanjo hujambo! Baada ya kusoma makala kuhusu Kwanzaa ninegependa kukuuliza kuhusu Kwanzaa jinsi unavyoiona ukiwa Mwafrika na Mwsahili. Nimetazama desturi hii kwa miaka kadhaa nikiwa mbali nikashangaa. Kwangu ilikuwa wazi ya kwamba sherehe hii haina kitu cha kiafrika ndani yake. Wala Afrika ya mashariki wa magharibi nimesikia ya kwamba kuna sikukuu ya mavuno wakati wa Disemba.
Kiswahili wanachotumia - basi naiona mtandaoni tu. Lakini kama ningemjibu mtu anayenisalimu "Habari gani" kwa maneno kama "kuumba" sijui angeniangalia namna gani.. Ama ataona nimesahau lugha au atajiuliza kama nimelewa. Wanaweka mahindi wakiita "muhindi" (sina neno kuhusu mahindi - imekuwa kiafrika sawa jinsi kiazi imekuwa kiingereza au kijerumani ingawa zote zimetoka Amerika ya Kusini, hata kama Wachagga na Waganda wasingekubali kamwe :-)) - ila tu lugha bovu). Unajua wewe mahali Afrika penye sherehe ya "matunda ya kwanza"???
Kwangu imeonekana kama sherehe ya kisintetiki yaani isiyo ya asili kabisa. Ni kama ndoto nyingine tena juu ya Afrika: Waingereza wanaota ndoto zao za "Out of Africa", karne zilizopita wataalamu wa Ulaya walikuwa na ndoto hizi za "Washenzi watukufu". Afrika ilikuwa na bado ni mara nyingi kama skrini ya filamu watu wanapotupa picha zilizomo kichwani mwao. Lakini si Afrika yenyewe.
Kwa upande mwingine nimefikiri basi si kitu kibaya kama watu wanatafuta habari za Kiswahili hata kama njia ni potovu. Ikisaidia kueneza kwa lugha ya Kiswahili nifunge macho? (Juzi nimepita mahali mtandaoni wanapotaja majina kwa ajili ya watoto wakidai ni ya Kiswahili - taz. http://www.babynology.com/swahili/baby-names-boy_M_100.html - natumaini ya kwamba kuna matokeo mazuri zaidi ya upendo ule wa Kiamerika wa lugha kuliko orodha hii!)
Juzi tu nimeona mara ya kwanza habari za huyu Karenga kuwa jina lake ni Ron Everett amekuwa na historia mbaya asiyopenda kukubali. Umewahi kukutana naye? Ameanza kujifunza Kiswahili siku hizi? Kujiita "Maulana" ili watu wote Marekani wanaamini ni neno la Kiswahili kwa ajili ya "mwalimu" ni ajabu nyingine kwangu.
Kwa hiyo - ningependa kusikia mawazo yako kweli! --Kipala 17:05, 8 Januari 2006 (UTC) (Nanakili haya kwenye majidiliano ya "Kwanzaa" - labda wenzetu wengine wana neno pia)
[edit] Kalenda ya Juliasi
Ndesanjo, nimeona matatizo na makala ya Kalenda.. Tafadhali angalia: http://sw.wikipedia.org/wiki/Talk:Kalenda_ya_Juliasi --Kipala 21:05, 19 Aprili 2006 (UTC)
[edit] Tuzo ya Nobel/Nobel
Ndesanjo, hujambo? Vema kukuona tena ulipotea kweli. Ombi: wakati wa kusahihisha tukumbuke viungo! "Tuzo ya Nobel" ilikuwa kiungo - "Nobeli" imekata kiungo. Ingekuwa vema kama ama unasahihisha viungo vyote au kukirudisha. --Kipala 12:21, 24 Juni 2006 (UTC)
- Narudia ombi la Kipala: Kwa vile umebadilisha herufi za viungo, umekata viungo hivyo. Sasa nimeongeza viungo vitano kwa tuzo za Nobel. Ukumbuke mara ijayo kuongeza viungo ambavyo herufi zake umevibadilisha. Asante! -- Oliver Stegen 08:47, 14 Agosti 2006 (UTC)
[edit] jambo
hujambo bwana? habari gani? it's mike/gozar from Wikimania 2006 checking in (apparently i had an account registered on here already). anyways, i may at some point add images to existing articles or make basic starts for others. probably country pages or those from the "articles every wikipedia should have" list...if i can find it! are you still in boston or have you moved on? kwa heri na asante.--Gozar 00:42, 10 Agosti 2006 (UTC)
[edit] mawasiliano na anwani
Ndesanjo, habari yako? Uliniomba nikutumie anwani yangu kupitia baruapepe. Je, umeipata? Sijasikia kutoka kwako. Wasalaam, Oliver Stegen 10:54, 2 Septemba 2006 (UTC)
[edit] Kutafuta maneno - Kuunda templeti
Ndesanjo, naomba msaada wako pamoja na Waswahili wengine. Niko kwenye makala za kijiografia / jiolojia nikiona tatizo la kuchagua maneno.
Kwa sasa nahitaji maneno kwa kutaja tabaka mbalimbali ya muundo wa dunia. Tatizo ni ya kwamba Kamusi ya KAST haionyeshi maneno ya kutosha. Je una ushauri kwa yafuatayo:
- crust - gamba la nje ? (KAST inataja "ganda" - lakini haina neno la "mantle")
- mantle (inner & outer) - ganda la dunia? (ya nje na ya ndani)
- core (inner & outer) - KAST inataja "masoka" (niliweka "kiini" kabla ya kuangalia kwenye KAST - natumaini Mswahili wa kawaida ameshasahau maana ya masoko=pepo mbaya) - nifuate KAST
Kwa hiyo nisaidie kati ya "gamba" na "ganda". Nikitumia ganda kwa sehemu ya nje kabisa ambayo ni imara imepoa (ile tunapoishi) nitumiaje kwa "mantle"? (KAST hawana kitu kile)
Lugha nyingi hutumia neno lilelile "mantle" - Warusi, Wapoland n.k. wameitafsiri tu - je nikichukua "johoo" ?? au "koti" ?? Waturuki wamepokea neno la Kiitalia/Kifaransa "manto" (nijaribu ile?? Kuazima kutoka nje si aibu)
Naona vema kuwa na templeti ya kuonyesha: "Makala hii inatumia neno ambalo matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotaja. Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao."
Je, unaonaje?? --Kipala 21:02, 2 Septemba 2006 (UTC)
Maswali magumu Kipala. Unaonaje nikiweka maswali haya pale kwenye kamusi hai mtandaoni? Binafsi ninapendelea "gamba" zaidi ya "ganda." Na "kiini" zaidi ya "masoka". Sioni ubaya kwenye kuazima neno na hivyo kutumia "manto." Unaonaje tukiuliza? --Ndesanjo
-
- Ni vizuri ukiuliza. Labda itawavuta wengine katika mradi huu. "Koti" unaonaje? Vipi wazo la Templeti na maneno yake? --Kipala 21:53, 2 Septemba 2006 (UTC)
Nilisahau kuhusu templeti. Ni wazo zuri sana. Tafadhali fanya.Itasaidia kwa kazi nyingine zinazoendana na hii unayoandika sasa. -Ndesanjo 2 Septemba 2006
[edit] Kumasi
Ndesanjo, asante kwa kunyosha Kiswahili changu! Miaka ya Nairobi imeniharibu!!! Kubaya mingi!! Lakini kiti kile cha Asantehene: je siyo "kigoda" huwa na miguu mitatu?? Muundo wa viti vya Ghana ni tofauti! Sina uhakika kinaitwa nini kwa Kiswahili hivyo nimetumia "kikalio". Angalia picha hapa: [[2]] --Kipala 20:40, 3 Septemba 2006 (UTC)
-
- Nilisahau kuwa kile hakina miguu kama ile ya kigoda, ni sawa tuiite kikalio. Ngoja nibadili.--Ndesanjo
[edit] Misitu na jangwa
Ndesanjo, umependekeza jamii: Vita vya msituni Afrika. Labda utafute jina nzuri zaidi. Nisipokosei vita ya POLISARIO au vita za Watuareg katika Sahara ni jambo lilelile - ila tu wanapigana jangwani pasipo na msitu kabisa. (Kwa Savimbi na Kony/LRA pekee ingekuwa sawa.) --Kipala 11:23, 11 Septemba 2006 (UTC)