Siku ya wapendanao

From Wikipedia

Siku ya wapendanao ni siku kuu hii huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14/2 ya kila mwaka (Valentine Day). Historia yake imeanzia karne ya 3 huko ROMA ambapo alikuwapo mtakatifu valentine au valentinus. Mtawala wakati huo alikuwa CLAUDIA WA PILI yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyeoa wala kuwa na familia (kapera). Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa askari. Mtakatifu valintine alipinga jambo hili hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme claudia alipopata habari hizi aliamuru kukamatwa kwa valentine na kuuwawa. Akiwa gerezani aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza za valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani, mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya (From your Valentine). Toka hapa valentine anakumbukwa kama mtetezi wawapendanao na siku hii kuadhimishwa kote duniani.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Siku ya wapendanao" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Siku ya wapendanao kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.