Jumuiya ya Afrika ya Mashariki

From Wikipedia

Nchi tatu za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki
Enlarge
Nchi tatu za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki

Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (East African Community - EAC) ni ushirikiano kati ya nchi za Afrika ya Mashariki hasa Kenya, Uganda na Tanzania.

Jumuiya hii imepatikana mara mbili katika historia:

Contents

[edit] Jumuiya ya kwanza

Nchi tatu za Afrika ya Mashariki zilizokuwa chini ya utawala wa Uingereza zilianza uhuru wao kwa ushirikiano wa karibu uliorithiwa kutokana na utawala wa pamoja wa kikoloni. Baada ya kupata uhuru 1961 nchi tatu ziliunda Mamlaka ya Huduma za Pamoja za Afrika ya Mashariki (East African Common Services Organisation – EACSO).

Ushirikiano ulihusu fedha (East African Shilling), forodha (Customs Union), huduma za reli (East African Railway), ndege (East African Airways), mabandari, posta na simu na elimu ya juu (Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki chenye kampasi Makerere, Daressalaam na Nairobi). Mkataba ulilenga pia kwa mahakama kuu ya pamoja na siasa ya kiuchumi ya soko la pamoja. Haya yote yalitakiwa kuwa chini ya Bunge la Afrika ya Mashariki.

Tangu 1965 umoja huu ulianza kurudi nyuma kila nchi ilianzisha pesa yake. Mwaka 1967 nchi tatu zilijaribu upya kuimarisha umoja wao kwa Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wakiita umoja wao „Jumuiya ya Afrika ya Mashariki“ ikiwa makao makuu ndipo Arusha.

Lakini mielekeo ya nchi zote tatu zilitofautiana mno Kenya ikiendelea kwa njia ya kipebari lakini Tanzania ilijaribu kujenga Ujamaa (usoshialisti) kuanzia mw. 1967. Uganda uliingia katika kipindi cha udikteta kali ya Idi Amini aliyeharibu uhusiana na majirani alipoanza kudai sehemu za maeneo yao.

Hivyo mwaka 1977 Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ilikuwa imekwisha kufanya kazi yoyote na 1983 ilifutwa rasmi. Mali iliyobaki iligawanywa kati ya nchi zote tatu.

[edit] Kufufuka kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki tangu 1993

Tangu miaka ya 1990 majaribio ya kunjenga umoja mpya yalionekana tena. Maraisi Moi wa Kenya, Mwinyi wa Tanzania, and Museveni wa Uganda walipatana Mkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki huko Arusha, Tanzania, tar. 30-11-1993.

Jumuiya mpya ya Afrika ya Mashariki ilianzishwa Januari 2001 huko Arusha – Tanzania penye makao makuu ya jumuiya hii. Mkataba wa 2004 uliweka msingi wa Umoja wa Forodha ulioanzishwa 2005.

Kuna tena Bunge la Afrika ya Mashariki linalojumuisha wabunge waliochaguliwa na bunge tatu za nchi wanachama.

Pia Mahakama Kuu ya Afrika ya Mashariki imeundwa upya.

Kuna mipango kuwa tena na pesa yapamoja kuanzia mwaka 2009.


[edit] Nchi wanachama

Burundi na Rwanda zinategemea kujiunga mwaka 2006.


[edit] Viungo vya Nje

Lugha nyingine