Kenya (mlima)

From Wikipedia

Mlima Kenya
Enlarge
Mlima Kenya

Mlima Kenya ndio mlima mrefu kuliko yote nchini Kenya. Mlima huu ambao hasa wenyeji waliuita Kirinyaga, una urefu wa mita 5,199. Ndio volkeno iliyozimika ikikadiriwa ya kwamba mlipuko wake wa mwisho ulitokea mnamo miaka milioni 2.6 hadi 3.1 iliyopita.

Kelele zake za juu zinaitwa Batian (5,199 m), Nelion (5,188 m) na Lenana (4,985 m). Kuna barafuto nane mlimani lakini zinapungua kila mwaka kutokana na kupanda kwa halijoto duniani na kupungukiwa kwa usimbishaji kwa sababu ya kukatwa kwa miti mingi.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Kenya (mlima)" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Kenya (mlima) kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.