Getrude Mongella

From Wikipedia

Getrude Mongella ni Rais wa Bunge la Umoja wa Afrika. Getrude alizaliwa mwaka 1954 katika kisiwa cha Ukerewe katika mkoa wa Mwanza (Tanzania). Baba yake, Mzee Patrice Magologozi alikuwa ni fundi seremala na mwashi na mama yake, Bibi Nambona, alikuwa ni mkulima.

Getrude Mongela ameshika nyadhifa mbalimbali za kitaifa na kimataifa. Mwaka 1993-95 alikuwa ni Katibu Mkuu wa Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya Wanawake, amewahi kuwa balozi India (1991-93), Waziri Asiye na Wizara Maalum, Waziri wa Ardhi, Maliasili na Utalii, mshauri maalum wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni, n.k.

Lugha nyingine