Senegal (mto)
From Wikipedia
Mto wa Senegal | |
---|---|
|
|
Chanzo | maungano ya mito ya Bafing na Bakoyé mjini Bafoulabé. |
Mdomo | {{{mdomo}}} |
Nchi | Guinea, Mali, Mauretania, Senegal |
Urefu | 1,790 km (2.272 km pamoja na Bafing) |
Kimo cha chanzo | 750 m |
Mkondo | 640 m³/s |
Eneo la beseni | 483,181 km² |
Mto wa Senegal ni kati ya mito mirefu ya Afrika ukiwa na urefu wa kilometa 2272 pamoja na tawimto mrefu wa Bafing. Mto Senegal wenyewe unaanza karibu na mji wa Bafoulabe (Mali) kwenye maungano ya mito miwili ya Bafing na Bakoye ambayo yote ina chanzo huko Guinea.
Urefu wa mto Senegal ni mpaka kati ya Mauretania na Senegal. Senegal ikikaribia bahari ya Atlantiki inafika kwenye kisiwa cha St. Louis halafu inageukia kusini. Sasa inafuata pwani la bahari ikitengwa na Atlantiki kwa kanda nyembamba ya mchanga tu hadi kuingia bahari ya Atlantiki.
Beseni ya Senegal ni kilometa za mraba 483,181. Tawimito muhimu ni Faleme, Karakoro na Gorgol.
Mali, Mauritania, Senegal na Guinea zimeshirikiana katika mamlaka ya beseni ya mto wa Senegal (Organisation pour la mise en valeur du fleuve Sénégal - OMVS).