Roma
From Wikipedia
"Roma" ni jina la mji wa Roma (mji mkuu wa Italia) ama jina la dola la Roma lililokuwa dola kubwa zamani.
Roma ni umbo la jina katika Kilatini na Kiitalia; imekuwa kawaida katika Kiswahili cha kisasa. "Rumi" ilikuwa kawaida katika Kiswahili cha zamani kutokana na kawaida ya lugha ya Kiarabu (الرُّومُ ar-Rūm). Matoleo ya Biblia ya "Union Version" iliyochapishwa tangu 1952 hutumia "Rumi", "Warumi". Tafsiri ya Biblia ya Kiswahili cha Kisasa hutumia "Roma", "Waroma".
- Mji wa Roma, jina la mji mkuu wa nchi ya Italia
- Dola la Roma, dola kubwa katika eneo la Mediteraneo (Ulaya, Asia ya Magharibi, Afrika ya Kaskazini) mnamo miaka 2100-1600 iliyopita. Limeendelea katika Dola ya Roma ya Mashariki au Bizanti hadi mwaka 1453 b.K.
- Roma ilikuwa jina la mungu wa kike katika dini ya Roma ya Kale
- Miji mingine inayoitwa kwa jina la "Roma" iko Australia, Ecuador na Marekani; pia eneo ndani ya mji wa Mexiko.
- Kutokana na jina la mji yamepatikana majina ya:
- Roma, meli ya kijeshi ya Italia;
- Roma ni jina la filamu mbalimbali;
- Roma ya Kale