Visiwa vya Virgin vya Marekani
From Wikipedia
Visiwa vya Virgin vya Marekani (United States Virgin Islands) ni visiwa katika Bahari ya Karibi ambavyo ni visiwa chini ya Marekani, wakazi ni raia wa Marekani lakini hawashiriki katika uchaguzi wa Rais wala wa bunge la Washington DC.
Ni hasa visiwa 4 vya St. Thomas, St. John, St. Croix na Kisiwa cha Maji (Water Island) pamoja na visiwa vingi vidogo.
Eneo lao kwa jumla ni 346.36 km². Sensa ya mwaka 2002 ilihesabu wakazi 108,612.
Visiwa hivi ni sehemu ya pekee ya Marekani ambako magari yanatembea upande wa kushoto ya barabara.
Visiwa vilikuwa koloni ya Denmark vikauzwa 17 Januari 1917 kwa Marekani.