Hugh Masekela

From Wikipedia

Hugh Masekela (alizaliwa 4 Aprili, 1939) ni mpulizaji mashuhuri wa tarumbeta wa Muziki wa Jazz. Alizaliwa mji wa [[Wilbank], Afrika ya Kusini. Hugh Masekela anafahamika ulimwenguni kote kwa aina ya kupiga Jazz la mtindo wa Afri Jazz na hasa upulizaji wake wa tarumbeta; uongozi wa bendi ya muziki; mtunzi na muandishi mahiri wa mashairi ya muziki. Masekela alijifunza kupuliza tarumbeta akiwa shuleni na mwalimu wake ni Padri Trevor Huddleston. Padri Trevor alikuwa ni mkuu wa shule yao Huddleston. Alifanya ziara New York, Marekani ambako alikutana na msanii maarufu wa kimarekani Louis Armstrong na aliporudi Afrika ya Kusini alibeba tarumbeta alizopewa na Armstrong ambazo zilimzindua Masekela na kuanza kufahamika.

Akiwa na umri wa miaka ishirini Masekela alikuwa akitumbuiza muziki wa aina tofauti, hasa wa Jazz; Bebop; Funk na Afrobeat wakati huo alikuwa na kundi la Jazz Epistles kundi hili lilikuwa na wasanii maarufu kama mpiga kinanda mahiri Abdillah Ibrahim. Mwaka 1960 Masekela alikwenda London Uingereza ambako alijiunga na shule ya muziki ya Guildhall School of Music na baadaye alikwenda New York, Marekani ambako alisoma katika mji wa Manhattan. Mwaka 1962 alitoa albamu yake ya kwanza iitwayo Trumpet Africa. Miaka miwili baadaye alitoa nyingine iitwayo The Americanisation of Ooga Booga ambayo ilitamba mpaka kushika chati, hasa baada ya kupigwa na kituo kimoja cha radio cha mjini California.

Kwenye miaka ya tisini Masekela alitoa albamu zifuatazo, (1992) Beatin' around de bush; (1993) Hope; (1995) Johannesburg; (1995) Notes of life; (1997) Black to the future; (1999) Sixty; (2003) Time na (2005) Rivival. Mpaka kufikia Agosti 2000 alikuwa ameuza nakala 50,000 na kumfanya apate tuzo ya Platinum,]. Hugh ameshirikiana na wasanii kama Miriam Makeba wa Afrika ya kusini na Paul Simon wa Marekani kwenye albamu ya Graceland. Tarumbeta lake limesikika zaidi kwenye wimbo wa Gumboots na Diamond in the sole of her shoes.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Hugh Masekela" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Hugh Masekela kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.