Edward Ngoyai Lowasa
From Wikipedia
Edward Ngoyayi Lowasa (*1953) ni waziri mkuu wa kumi wa Tanzania. Amechaguliwa tar. 30 Desemba, 2005.
Lowassa ni mwenyeji wa Monduli katika Mkoa wa Arusha. Alisoma digrii ya kwanza ya tamthilia kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam halafu digrii ya pili katika sayansi kwenye Chuo Kikuu cha Bath (Uingereza).
Lowassa ameshika vyeo mbalimbali katika serikali ya Tanzania kama vile:
- Waziri wa Maji na Mifugo (2000 - 2005)
- Waziri wa ardhi na makazi (1993 - 1995)
- Waziri mdogo wa haki na mambo ya bunge katika ofisi ya Makamu wa Rais (1990-1993)
- Mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (1989 - 1990)
- Waziri mdogo wa mazingira na mapambano dhii ya umasini katika ofisi ya Makamu wa Rais (1988-2000)
- Mbunge wa Monduli tangu 1990