Omdurman
From Wikipedia
Omdurman (au: Omdourman, Kar: أم درمان Umm Durmān ) ni mji mkubwa kabisa nchini Sudan kando la mto Nile ikitazama mji mkuu Khartoum. Pamoja na Khartoum na Bahri ni mji mmoja kubwa sana unaounganishwa kwa madaraja kadhaa.
Ina wakazi wanaokadiriwa kufikia karibu milioni 3.
[edit] Historia
Mji ulianzishwa na Muhammad Ahmad ibn Abd Allah Al-Mahdi mwaka 1885. Baada ya jeshi lake kuteka Khartoum katika vita dhidi ya Misri na gavana yake Gordon Mahdi Muhammad hakutaka kukaa kwenye "mji wa makafiri" akajenga mji mpya wa Omdurman "mji wa waumini" ng'ambo ya mto Nile uliokuwa mji mkuu wa dola la mahdi 1885 - 1898. Wakati ule Omdurman ilikuwa tayari na wakazi 150,000.
Waingereza walipoteka Sudan mwaka 1898 Omdurman ilirudi nyuma lakini miaka ya nyuma ilikua tena kupita Khartoum kutokana na kufika kwa wakimbizi wengi mjini kutoka nchi jirani kama Chad, Eritrea, Ethiopia na Uganda, pia wakimbizi kutoka vita ya Sudan ya Kusini. Wakimbizi hawa walijenga mitaa mikubwa ya vibanda.
[edit] Utamaduni na elimu
Omdurman ina vyuo vikuu kadhaa. Kumbukumbu ya kihistoria muhimu ni kaburi la Mahdi.