Marijani Rajab
From Wikipedia
Marijan Rajab ni mmoja wa wanamuziki kutoka Tanzania ambaye atakumbukwa daima. Marijani alikuwa ni kiongozi wa bendi ya The Safari Tripers, na baadaye Dar International Orchestra. Uwezo wa Marijan kuandika tungo zinazogusa maisha ya kila siku kama vile mapenzi, msiba, wivu, ufukara, n.k. na kuziimba kwa sauti ya pekee ulimpa jina "jabali la muziki." Nyimbo maarufu alizoandika na kuimba Marijan ni pamoja na Georgina, Mayasa, Zuwena, Uzuri wa asili, Mateso, Masudi, na Mwanameka.