Kasoko

From Wikipedia

Kasoko ni shimo kwenye ardhi kutokana na mlipuko au mshtuko wa kugongwa na gimba.

Kasoko hutokea kutokana na

  • mlipuko wa bomu iliyolipuka ndani ya ardhi au juu ya uso wa ardhi
  • mgongano wa gimba kubwa ardhini kwa mfano meteoridi
  • Kasoko ya volkeno: shimo ambako lava inatoka nje

Kasoko kubwa zaidi duniani zilisababishwa na meteoridi zilizogonga dunia yetu. Kasoko kubwa iliyojulikana hadi 2006 ilikuwa kasoko ya Vredefort nchini (Afrika Kusini) yenye umbo la yai ya urefu wa 320 km na upana wa 180 km.

Mwaka 2006 wataalamu waligundua kasoko kubwa zaidi yenye kipenyo cha 500 km huko Antarktika katika picha zilizopigwa angani. Iko chini ya barafu ya Antarktika katika eneo la Wilkes Land inatajwa kwa kifupi cha WLIC (kiing.: Wilkes Land impact crater). Kasoko ya WLIC inaaminiwa imesababishwa na meteoridi yenye kipenyo cha takriban 5 km.

Ukarasa huu una maelezo ya maana ili kutofautisha nia mbalimbali zinazolengwa na neno moja. Chagua maana uliyoikusudi.

Maelezo katika ukarasa huu yawe mafupi, na kwa kila maana kuwe na kiungo kimoja tu ambacho kiunge ukarasa kuhusu nia yenye maana hii. Ukiwa umefika hapa kwa kutumia kiungo katika makala nyingine, tafadhali badalisha kiungo kile kiunge makala iliyokusudiwa moja kwa moja.