Chama cha Mapinduzi

From Wikipedia

Chama cha Mapinduzi (CCM) ni chama tawala nchini Tanzania. CCM ilizaliwa Januari 1977 baada ya kuungana kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU), chama kilichokuwa kikitawala Tanganyika, na Afro-Shiraz Party (ASP), chama tawala cha Zanzibar wakati huo. Chama cha Mapinduzi kilikuwa kikiongozwa na Mwalimu Nyerere na Afro-Shiraz Party kilikuwa chini ya Amaan Karume.

Contents

[edit] Itikadi

Kwa miaka mingi CCM ilikuwa ikifuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Itikadi hii ilipewa nguvu za kisera mwaka 1967 lilipotangazwa Azimio la Arusha. Kutokana na azimio hilo uchumi uliwekwa mikononi mwa umma. Itikadi hii pia ilisisitiza umuhimu wa kuishi pamoja hasa katika vijiji vya Ujamaa.

[edit] Uchaguzi

CCM imekuwa ikishinda chaguzi za Urais toka mfumo wa vyama vingi uliporejeshwa nchini Tanzania. Chama hicho kimekuwa pia kikipata idadi kubwa ya wabunge wa Bunge la Muungano na Baraza la Wawakilishi. Chaguzi za vyama vingi Tanzania baada ya kurejeshwa kwa mfumo huo zilifanyika mwaka 1995, 2000, na 2005.

[edit] Uongozi

Katika historia ya CCM kumekuwa na wenyeviti wanne: Mwalimu Nyerere, Mwenyekiti wake wa kwanza toka 1977 hadi 1990, Ali Hassan Mwinyi toka 1990 - 1996, na Benjamin Mkapa 1995-2005, na Jakaya Kikwete, 2006 -?

[edit] Viungo vya nje