Bamba la Afrika

From Wikipedia

Bamba la Afrika (nyekundu-njano) kati ya mabamba gandunia ya dunia yetu
Enlarge
Bamba la Afrika (nyekundu-njano) kati ya mabamba gandunia ya dunia yetu
Ramani ya Afrika ya Mashariki inayoonyesha volkeno kadhaa (pembetatu nyekundu) na pembetatu ya Afar - eneo la kuachana kwa bamba la Uarabuni na bamba la Afrika linalojipasua hapa kuwa bamba la Afrika ya Kinubia na la Afrika ya kisomalia.
Enlarge
Ramani ya Afrika ya Mashariki inayoonyesha volkeno kadhaa (pembetatu nyekundu) na pembetatu ya Afar - eneo la kuachana kwa bamba la Uarabuni na bamba la Afrika linalojipasua hapa kuwa bamba la Afrika ya Kinubia na la Afrika ya kisomalia.

Bamba la Afrika ni kati ya mabamba makubwa ya gandunia ya dunia yetu. Lipo chini ya bara la Afrika na chini ya sehemu za bahari zinazopakana nalo yaani tako la bara.

Bamba hili limepakana na bamba la Ulaya-Asia, bamba la Uarabuni, bamba la Uhindi, bamba la Australia, bamba la Antaktika. Inawezekana ya kwamba limepakana na mabamba madogo mengine yasiyoeleweka bado.

Bamba la Afrika lina mwendo wa kuelekea kaskazini unaopimwa kuwa 2.15 cm kila mwaka. Kwa mkasi huu bara la Afrika litagusana na Hispania ya Kusini baada ya miaka 650,000 na kufunga mlango wa bahari ya Gibraltar hivyo kufunga Mediteranea na kuifanya kuwa ziwa.

Bamba la Afrika yenyewe liko katika mwendo wa kupasuliwa kwenye mstari wa ufa la Afrika ya Mashariki kutoka Eritrea kupitia Ethiopia, Kenya, Tanzania, Malawi na mwishowe katika Msumbiji. Sehemu mbili za bamba la Afrika huitwa na wataalamu bamba la Afrika ya Kinubia na la Afrika ya kisomalia.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Bamba la Afrika" inatumia neno ambalo matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazionyeshi maana inayohitajiwa.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Bamba la Afrika" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Bamba la Afrika kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.