Wachagga
From Wikipedia
Wachagga ni kabila la watu wenye asili ya Kibantu wanaoishi kaskazini mwa Tanzania chini ya mlima Kilimanjaro, mkoani Kilimanjaro. Shughuli kubwa ya Wachagga ni biashara na kilimo. Wachagga hulima mazao ya chakula kama vile mahindi, maharagwe, na ndizi, na pia mazao ya biashara kama vile kahawa.
Wachagga wana historia ndefu ya asili yao na maingiliano yao na makabila mengine na ndiyo sababu lugha yao, Kichagga, inabadilika kuanzia unapotoka Tarakea, Rombo magharibi ya Kilimanjaro mpaka unapofika Siha, Machame magharibi mwa Kilimanjaro. Kutokana na tofauti hizo Kichagga kimegawanyika katika makundi ya Kichagga cha Rombo, Marangu, Old Moshi, Kibosho, na Machame. Baadhi ya wachagga walihamia sehemu za Meru Arusha na kuchanganyikana na waarusha, lugha yao ilibadilika kidogo na kuwa Ki-meru. Kwa sababu hii wameru wanasikilizana sana na wachagga wa machame ingawa lafudhi zao zinatofautiana desturi na mila zao ziko karibu sana.
Wachagga wanajulikana kwa uwezo wao mkubwa wa kufanya biashara na pia kilimo. Moshi ni maeneo ya mwanzo ambayo Wamisionari wa Kikristo walijenga makanisa na shule. Sababu hii imefanya Wachagga kuwa kati ya kabila lenye watu wengi walio na elimu ya kisasa na mkoa wa Kilimanjaro kuwa unaongoza kwa idadi ya shule nchini Tanzania.
Chakula kikuu cha Wachagga ni ndizi. Wachagga hutengeneza pombe maarufu iitwayo mbege. Mbege hutengenezwa kwa kutumia ndizi mbivu, maji, na ulezi.
Wachagga ni kabila tatu kwa ukubwa nchini Tanzania. Takwimu za mwaka 2003 zinaonyesha kuwa idadi ya Wachagga mkoani Kilimanjaro ni 200,000
Familia maarufu za kichagga nchini Tanzania ni kama Urassa,Nkya,Temu,Mariki,Tarimo,Laswai,na kadhalika. Pia inasemekana kuwa,Wachagga wengi hupenda kurudi nyumbani kipindi cha krismasi,ikiwa ni kuwatembelea wazazi wao,rafiki,au ndugu.
[edit] Viungo vya nje
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Wachagga" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Wachagga kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |