Visiwa vya Kanari

From Wikipedia

Visiwa vya Kanari na Hispania
Enlarge
Visiwa vya Kanari na Hispania

Visiwa vya Kanari (Kihispania: Islas Canarias) ni funguvisiwa ya Afrika ya Kaskazini katika bahari ya Atlantiki. Kisiasa ni sehemu ya ufalme wa Hispania. Viko baharini 150 km upande wa magharibi ya Moroko. Umbali na Hispania ni masaa mawili kwa ndege.


Contents

[edit] Utawala

Mapa de las Islas Canarias.
Enlarge
Mapa de las Islas Canarias.

Kisiasa visiwa ni kati ya maeneo ya kujitawala ndani ya ufalme wa Hispania.

Visiwa vikubwa ni saba:

El Hierro, La Gomera, La Palma na Tenerife ambavyo ni mkoa wa Santa Cruz de Tenerife,

halafu Gran Canaria, Fuerteventura na Lanzarote ambavyo ni mkoa wa Las Palmas,

tena visiwa vidogo sita vya Alegranza, Kisiwa cha Lobos, La Graciosa, Montaña Clara, Roque del Este na Roque del Oeste, vyote vya Las Palmas.

Miji mikuu ni Las Palmas de Gran Canaria na Santa Cruz de Tenerife.

Makao ya mkuu wa serikali ya eneo huhamahama kati ya miji hii miwili kila baada ya miaka minne.

[edit] Wakazi

Jumla ya wakazi kufuatana na sensa ya mwaka 2005 ni 1,968,280. Mkoa wa Las Palmas una wakazi 1.011.928 katika tarafa 33, mkoa wa Santa Cruz de Tenerife una watu 956.352 katika tarafa 52.

Miji mikubwa ni Las Palmas de Gran Canaria (wakazi 378.628), Santa Cruz de Tenerife (wakazi 221.567), San Cristóbal de la Laguna (wakazi 141.627) na Telde (wakazi 96.547).

Idadi ya wakazi wa visiwa ni kama ifuatayo:

  • Tenerife - 838.877
  • Gran Canaria - 802.247
  • Lanzarote - 123.039
  • Fuerteventura - 86.642
  • La Palma - 85.252
  • La Gomera - 21.746
  • El Hierro - 10.477


[edit] Historia

Visiwa vya Kanari vilitembelewa zamani na wasafiri Wafinisia, Wagiriki na Waroma, baadaye na Waarabu. Katika Ulaya visiwa vilisahauliwa hadi mnamo mwaka 1400.

Viisiwa vilikaliwa na wazalendo walioitwa Guancha na Wahispania walipofika Kanari. Hakuna uhakika kuhusu asili yao. Wataalamu wengine hufikiri walikuwa Waberber. Wengine husema walikuwa wafungwa walioachiwa huru visiwani wakati wa Dola la Roma.

Wakati wa kufika kwa Wahispania kuanzia mwaka 1400 walikuwa na utamaduni bila chuma wanasemekana hawakujua usafiri wa bahari. Katika muda wa karne moja Wahispania walivamia visiwa na kukandamiza utamaduni wa wenyeji. Lugha yao imekwisha kabisa ingawa kuna bado majina ya mahali visiwani kutokana na lugha ya Kiguancha.

Baada ya Wahispania kufika Amerika Las Palmas ilikuwa bandari muhimu ya safari za Atlantiki.

Watalii mwambanoni Fuerteventura
Enlarge
Watalii mwambanoni Fuerteventura

[edit] Uchumi

Kutokana na uzuri wa nchi na hali ya hewa ambayo ni poa mwaka wote utalii imekuwa nguzo ya uchumi wa visiwa vya Kanari pamoja na kilimo cha mazao ya sokoni yanoyopelekwa Ulaya, hasa ndizi na tumbaku.



Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia