Victoria (ziwa)

From Wikipedia

Ziwa la Viktoria Nyanza
Ziwa Viktoria Nyanza jinsi inavyoonekana kutoka angani
Ziwa Viktoria Nyanza jinsi inavyoonekana kutoka angani
Mahali Afrika ya Mashariki
Nchi zinazopakana Tanzania, Kenya na Uganda
Eneo la maji 68,100 km²
Kina ya chini 81 m
Mito inayoingia Kagera, Katonga, Nzoia
Mito inayotoka Nile
Kimo cha uwiano wa maji juu ya UB 1,134 m
Miji mikubwa ufukoni Kampala, Kisumu, Mwanza

Ziwa Victoria au Viktoria Nyanza ni ziwa kubwa Afrika, pia ni chanzo cha mto Nile, hili ni ziwa la pili kwa ukubwa Duniani. Ziwa la kwanza ni ziwa Superior ambalo lipo Amerika ya kaskazini, ziwa Victoria lipo futi 3,726 kutoka usawa wa bahari lina eneo la maili za mraba zaidi ya 26,000 maji ya ziwa Victoria yanamiminika kwenye mto Nile na kuelekea bahari ya Mediterenia kwa umbaili wa maili 4,000. Hata hivyo ziwa Victoria limekuwa ni kiunganisho na mpaka kwa nchi tatu za Afrika ya mashariki ambazo ni Tanzania; Kenya na Uganda.

[edit] Viungo vya Nje

Watersheds of Africa: A10 Nile | Lake Victoria


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Victoria (ziwa)" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Victoria (ziwa) kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.