Mkoa wa Kilimanjaro

From Wikipedia

Mkoa wa Kilimanjaro katika Tanzania
Enlarge
Mkoa wa Kilimanjaro katika Tanzania
Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro
Enlarge
Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro

Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 26 za Tanzania. Makao makuu ya mkoa huu ni Moshi. Mlima wa Kilimanjaro, mlima mkubwa kupita yote barani Afrika umo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Jina la mlima huu ndio limeupatia mkoa huu jina lake.

Mkoa wa Kilimanjaro umepakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa Kusini na mikoa ya Manyara na Arusha upande wa magharibi.

Kilimajaro kuna wakazi wapatao 1,381,149 (sensa ya mwaka 2002). [1]. Kabila kubwa ndio Wachagga. Makabila mengine mkoani humo ni Wapare na Wamasai

[edit] Wilaya

Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 6 ambazo ni: Rombo, Hai, Moshi Vijijini, Moshi Mjini, Mwanga na Same.

[edit] Marejeo


 
Mikoa ya Tanzania
Bandera Tanzania
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Iringa | Kagera | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Singida | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |
Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Mkoa wa Kilimanjaro" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Mkoa wa Kilimanjaro kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.

Lugha nyingine