Zanzibar (Jiji)
From Wikipedia
Jiji la Zanzibar ni mji mkubwa wa kisiwa cha Unguja na mji mkuu wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, pia ni wilaya katika Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi wa Tanzania.
Jiji lina wakazi 206,292 (sensa ya 2002).
Kitovu cha kihistoria ni Mji Mkongwe (Stone Town) ulioandikishwa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia" (World Heritage). Nyumba za Mji Mkongwe zilijengwa tangu 1830 wakati Sultani Sayyid Said alipohamisha mji mkuu wake kutoka Omani kuja Unguja. Kati ya majengo maarufu ni Beit al Ajaib (nyumba ya maajabu), boma la kale, Kanisa Kuu la Kianglikana kwenye mahali pa soko la watumwa na hasa nyumba nyingi za kihistoria za ghorofa zilizojengwa na famila za tabaka ya matajiri Waarabu zenye milango yenye mapambo mazuri.
Mji Mkongwe unapokea watalii wengi kila mwaka.
Mji wa kisasa umekua sana ngambo ya Mji Mkongwe.