Wanamichezo
From Wikipedia
MIKE TYSON: Mpiganaji wa ngumi za uzito wa juu duniani zinazotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBC). Ni bondia wa kwanza kuwahi kutwaa taji hilo akiwa na umri mdogo. Mike alizaliwa katika mji wa Brooklyn New York mwaka 1979. Alikuwa mtoto mtukutu akijihusisha na matukio ya uporaji mitaani. Alipelekwa katika shule ya kurekebisha tabia (Jela ya watoto) huko New York. Akiwa huko alionekana mwenye kipaji na mwalimu wa ngumi Mmarekani aitwaye Cus De Amato ambaye matunda yake mengine ni mwanamasumbwi aitwaye Floyd Petterson na kutwaa taji la ngumi 1956.