Belmopan

From Wikipedia

Mahali pa Belmopan nchini Belize
Enlarge
Mahali pa Belmopan nchini Belize
Jengo la Bunge la Belize mjini Belmopan
Enlarge
Jengo la Bunge la Belize mjini Belmopan

Belmopan ni mji mkuu wa Belize. Idadi ya wakazi ni takriban watu 15,000. Jina la mji liliundwa na maneno mawili ya "Belize" (=nchi) na "Mopan" ambayo ni mto wa karibu.

Belmopan iko kando la mto Belize kwenye 17°15′N 88°46′W takriban mita 76 juu ya UB. Ilichukua nafasi ya Belize City mji mkuu wa awali ulioharibika kabisa na dhoruba ya tufani mwaka 1961. Mji ulipangwa kwa ajili ya wakazi 40,000 lakini haikukua ipasavyo.

Pamoja na ofisi za serikali na bunge kuna pia chuo kikuu cha Belize.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Belmopan" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Belmopan kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.