Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani

From Wikipedia

Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani ni jina rasmi ya nchi ya Ujerumani tangu 3 Oktoba 1990.

Ujerumani, kanda za utawala wa washindi wa Vita Kuu ya Pili mw. 1946
Enlarge
Ujerumani, kanda za utawala wa washindi wa Vita Kuu ya Pili mw. 1946
Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani 1949 - 1990
Enlarge
Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani 1949 - 1990

Kati ya 1949 na 1991 ilikuwa jina la dola katika magharibi na kusini ya Ujerumani. Iliundwa katika maeneo ya kanda za utawala wa nchi washindi wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia Marekani, Uingereza na Ufaransa.

Dola hili lilijulikana pia kama "Ujerumani wa Magharibi". Wajerumani wengi hawakupenda jina hili kwa sababu katika lugha ya Kijerumani ni jina ni jina la kutaja eneo la magharibi la nchi hasa maeneo karibu na mto Rhine. Watu wa kusini na kaskazini kama wakazi wa Bavaria au Hamburg hawakujisikia kama "Wajerumani wa Magharibi".

Mji mkuu ulikuwa Bonn.

Kanda la Kirusi la Ujerumani ilikuwa dola la pili katika Ujerumani kwa jina la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani.