Jonas Savimbi

From Wikipedia

Jonas Malheiro Savimbi alikuwa ni kiongozi wa vita vya msituni nchini Angola. Savimbi alizaliwa 3 Agosti 1934 na kufariki 22 Februari 2002. Mwaka 1966 alianzisha vuguvugu la UNITA (kireno: União Nacional para a Independência Total de Angola).

Savimbi aliongoza UNITA iliyokuwa ikipata misaada toka serikali mbalimbali duniani ili kuiondoa madarakani serikali ya MPLA (kireno: Movimento Popular de Libertação de Angola - Partido do Trabalho). Savimbi alikuwa akipata misaada ya fedha na silaha toka serikali za Marekani, China, Afrika Kusini, Ivory Coast, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (wakati huo ikijulikana kama Zaire), Moroko, n.k. Serikali ya Angola ilikuwa ikipata misaada toka Urusi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani, Kuba, na Nicaragua.


[edit] Viungo vya nje

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Jonas Savimbi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Jonas Savimbi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.