Moravia

From Wikipedia

Bendera ya Moravia
Enlarge
Bendera ya Moravia
Moravia katika jamhuri ya Uceki
Enlarge
Moravia katika jamhuri ya Uceki

Moravia (Kiceki na Kislovakia: Morava; Kijerumani: Mähren; Kihungaria: Morvaország; Kipoland:Morawy) ni mkoa wa kihistoria katika mashariki ya Uceki. Jina limetokana na mto Morava.

Pamoja na Bohemia eneo la Moravia ni sehemu muhimu ya Uceki ambayo nii nchi iliyoanzishwa mwaka 1993 baada ya Slovakia kutoka katika Czechoslovakia.

Mji mkuu wa Moravia ni mji wa Brno (Kijerumani: Brünn).

Moravia ilikaliwa na makabila ya Waslavoni tangu karne ya 6. Katika karne ya tisa dola la Moravia ilikuwa himaya muhimu zaidi kati ya Waslavoni wa Ulaya. Mwanzo wa karne ya 10 himaya iliporomoka kati ya uenezaji wa Wajerumani upande wa magharibi na Wahungaria upande wa mashariki-kusini.

Katika kare zilizofuata Moravia ilikuwa chini ya athira ya Poland au Ujerumani ikaishia kuwa sehemu ya Dola Takatifu la Ujerumani na tangu 1437 chini ya utawala wa familia ya Habsburg.

Tangu 1918 Moravia ilikuwa jimbo la nchi ya Cekoslovakia, tangu 1993 ya Uceki.