Kibantu, lugha

From Wikipedia

Lugha za Kibantu ni kikundi cha mamia ya lugha za Kiafrika. Huzungumzwa hasa katika sehemu ya Kusini ya Bara la Afrika. Jumla ya wasemaji ni zaidi ya milioni 310. Wanapatikana kuanzia Kamerun ya Kusini, Gabun, Jamhuri zote mbili za Kongo, Uganda na Kenia halafu katika nchi zote kuelekea kusini.

Lugha za Kibantu zina sifa mbalimbali za pamoja. Kati ya sifa hizi za pamoja ni viambishi vya awali na ngeli za nomino.

Kutokana na sifa hizi wataalamu wa lugha wamekadiria ya kwamba asili ya lugha za Kibantu ilikuwepo katika maeneo ya Kamerun ya Kusini; kutoka huko wasemaji wa Kibantu asilia walihamia katika milenia ya pili k.K. Kongo hadi Zambia. Waliendelea kuhamahama na kupanuka hadi kufika maeneo yote walipo sasa. Sehemu kubwa ya maeneo ya wasemaji wa lugha za Kibantu zilikaliwa awali na wasemaji wa lugha za Khoikhoi. Wataalamu wamekadiria ya kwamba Wabantu walifaulu kunea kutokana na maarifa yao ya kilimo na hasa matumizi ya chuma katika zana za kilimo na pia silaha.

Kati ya lugha za Kibantu zinazotumika zaidi ni Kiswahili na Kilingala. Lugha zenye wasemaji wengi kama lugha ya kwanza ni Kizulu na Kishona.


Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Kibantu, lugha" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Kibantu, lugha kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.