Mkoa wa Kagera

From Wikipedia

Ramani ya mkoa wa Kagera
Enlarge
Ramani ya mkoa wa Kagera

Mkoa wa Kagera ni mkoa wa kaskazini-magharibi kabisa katika Tanzania. Jina lake linatokana na mto Kagera.

Mkoa wa Kagera umepakana na Burundi, Rwanda na Uganda upande wa Magharibi na Kaskazini. Upande wa Kusini umepakana na mikoa mengine ya Tanzania ya Kigoma, Shinyanga na Mwanza. Eneo lake ni 28,953 km² za nchi kavu na 11,885 km² za maji hasa ya Viktoria Nyanza, jumla 40,838 km².

Mkoa wa Kagera uko mnamo 1000 m juu ya uwiano wa bahari.

Makao makuu ya mkoa ni mji wa Bukoba.

Kuna wilaya tano za Bukoba, Muleba, Karagwe, Ngara na Biharamulo. Kuna halmashauri sita za Bukoba Mjini, Bukoba Vijijini, Karagwe, Muleba, Biharamulo na Ngara.

Sensa ya mw. 2003 imeonyesha idadi ya wakazi kuwa 2,003,888 inayoendelea kuongezeka asilimia 3.1% kwa mwaka.

[edit] External links


 
Mikoa ya Tanzania
Bandera Tanzania
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Iringa | Kagera | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Singida | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |