Jamestown (St. Helena)
From Wikipedia
Jamestown (wakazi 900) ni bandari na mji mkuu wa kisiwa na eneo la ng'ambo la Uingereza la Saint Helena katika bahari ya Atlantiki.
Mji ulianzishwa na Kampuni ya Kiingereza ya India ya Mashariki mwaka 1659. Miaka ya nyuma bandari ya Jamestown ilikuwa kituo muhimu cha safari za merikebu ya matanga kubwa. Wafanyabiashara walipeleka dhahabu yao hadi St. Helena kwa sababu kisiwa kilikuwa na sifa ya kuwa mahali pa usalama kwa kutunza dhahabu. Haya yote imepungua hadi kupotea kabisa. Leo hii kuna meli tu ya RMS St Helena inayofika takriban mara 2 kwa mwezi ikitumia siku 4-5 kwa ajili ya safari hadi Afrika Kusini. Idadi ya wakazi wa Jamestown imeendelea kupungua.
Mji mwenyewe ni hasa barabara moja yenye nyumba za aina ya ujenzi wa kikoloni cha Kiingereza.