Hans Krebs
From Wikipedia
Hans Adolf Krebs (25 Agosti, 1900 – 22 Novemba, 1981) alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Mwaka wa 1933, kwa vile wazazi wake walikuwa Wayahudi alilazimishwa kuhamia Uingereza. Hasa alichunguza athari za kikemia ndani ya chembe hai. Mwaka wa 1953, pamoja na Fritz Lipmann alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Tiba. Mwaka wa 1958 alipewa cheo cha “Sir” cha Uingereza.