Kamusi za Kiswahili

From Wikipedia

Kamusi za Kiswahili ni vyombo muhimu sana kwa kukuza na kuimarisha lugha. Kamusi zilianza kupatikana katika karne ya 19 BK. Waswahili wenyewe hawajulikani kuwa wametunga kamusi kabla wakati ule.

Contents

[edit] Ludwig Krapf

Kamusi ya kwanza inayojulikana ilitungwa mnamo 1848 na Ludwig Krapf huko Rabai Mpya / Mombasa (Kenya); ilikamilishwa na kutolewa kama "A Dictionary of the Suaheli language, London 1882".

[edit] Kamusi za kwanza

Wengine walioendelea kukusanya maneno na kutoa kamusi ni Askofu Mwanglikana Edward Steere (A handbook of the Swahili language: as spoken at Zanzibar. London: Bell & Daldy, 1870) na A. C. Madan (English-Swahili Dictionary, Oxford 1901 na Swahili-English Dictionary Oxford 1903).

Kamusi ya Kiswahili -Kijerumani zilipatikana mwaka 1890 na Büttner (Wörterbuch der Suaheli-Sprache, Berlin 1891) na mwaka 1911 wakati wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani na C. Velten (Suaheli Wörterbuch, Berlin 1910).

Kamusi ya Kiswahili - Kifaransa ilitolewa na Sacleux (Dictionnaire Francais-Souaheli, Paris 1891).

[edit] Kiswahili sanifu

Hadi mwanzo wa karne ya 20 Kiswahili kilipatikana katika lahaja zake tu. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza kamati iliundwa na serikali ya kikoloni kwa kusudi la kuunda Kiswahili sanifu kitakachotumiwa kote Afrika ya Mashariki. Kamusi mbili za "Inter-territorial Language (Swahili) committee to the East African Dependencies" zilitolewa mwaka 1939 zimechapishwa upya mara nyingi. Mhariri Mkuu wa kamati alikuwa katibu yake Frederick Johnson. Msingi wa kamusi hizi ulikuwa kazi ya Madan (taz. juu). Hivyo kamusi hizi hutajwa kama "Madan-Johnson".

[edit] Kiswahili tangu uhuru

Tangu kupatikana kwa uhuru wa nchi za Afrika ya Mashariki Kiswahili kiliendelea sana. Azimio la serikali ya Tanzania la kufanya Kiswahili kuwa lugha ya elimu katika shule za msingi lilianzisha masharti ya kutunga vitabu vya shule na kupanusha msamiati wa Kiswahili. Orodha za maneno zilitungwa kwa ajili ya masomo mbalimbali. TUKI katika Tanzania ilianza kuandaa kamusi mbalimbali hasa "Kamusi ya Kiswahili Sanifu" inayoeleza maana ya maneno kwa kutumia lugha yenyewe. Kamusi mbalimbali zilifuata.


[edit] Kamusi za maana zinazopatikana

Vifupi katika mabano si kawaida lakini vimeingizwa hapa kwa kusidi la kurahisisha marejeo katika makala za wikipedia.

Kiswahili - Kiswahili

  • Kamusi Ya Kiswahili sanifu (KKS). Dar es Salaam, Tanzania: Oxford University Press. 1981. (imetungwa na TUKI)
  • Bakhressa, Salim K. Kamusi ya manaa na matumizi (KMM). Nairobi, Kenya: Oxford University Press, 1992

Kiswahili - Kiingereza

  • Kamusi ya Kiswahili - Kiingereza (KKK) (imetungwa TUKI, Dar es Salaam 2001)
  • Kamusi Awali ya Sayansi na Tekinologia (KAST). Dar es Salaam, Tanzania: Ben & Co. Ltd., 1995.(imetungwa na TUKI)
  • Madan-Johnson, A Standard Swahili-English Dictionary (M-J SSE)(hutolewa na Oxford University Press, Nairobi & Dar es Salaam, 1939 na kuchapishwa upya mara nyingi)

Kiingereza - Kiswahili

  • English-Swahili Dictionary (ESD) (imetungwa na TUKI, Dar es Salaam 1996)
  • Madan-Johnson, A Standard English-Swahili Dictionary (M-J SES) (Oxford University Press, Nairobi & Dar es Salaam, 1939 na kuchapishwa upya mara nyingi)

Kamusi mtandaoni

Kiswahili - Kijerumani

  • Swahili-Deutsch, von Hildegard Höftmann, Irmtraud Herms (Langenscheidts Handwörterbuch München 2000, ISBN: 3468043902)
  • Deutsch-Swahili von Karsten Legere (Langenscheidts Handwörterbuch München 2000, ISBN: 3468043910)