Kofi Annan

From Wikipedia

Kofi Annan
Enlarge
Kofi Annan

Kofi Annan ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Amezaliwa mjini Kumasi (Ghana) tar. 8 Aprili, 1938.

Baada ya masomo ya uchumi alijiunga na huduma ya Umoja wa Mataifa mwaka 1962 katika WHO. 1974-1976 alifanya kazi Ghana halafu akarudi tena huduma ya UM. Akapanda ngazi kuwa Makamu wa Katibu Mkuu mhusika wa usalama aliwajibika kusimamia shughuli za wanajeshi walio chini ya UM.

Alihusika na vita ya Rwanda pia ya Yugoslavia ambako wanajeshi chini ya bendera ya UM walishirikiana.

1996 alichaguliwa kuwa Katibu Mkuuwa UM, akarudishwa cheo mwaka 2001.

Kofi Annan ameoa mara ya pili. Mke wake ni Msweden Nane Maria Annan. Ana watoto watatu.