Simon Bolivar

From Wikipedia

Simon Bolivar
Enlarge
Simon Bolivar

Simon Bolivar alikuwa mwanasiasa na mwanajeshi katika Amerika ya Kusini aliyeongoza mapambano dhidi ya ukoloni wa Hispania. Nchi mbalimbali humkumbuka kama baba wa taifa lao.

Alizaliwa 24 Julai 1783 mjini Caracas (wakati ule: Granada mpya, leo: Venezuela) akaaga dunia mjini Santa Marta (Kolombia) tar. 17 Desemba 1830.

Kama jemadari alishinda jeshi la Hispania kati ya 1810 na 1820.

Bolivar alikuwa kwa nyakati mbalimbali

  • rais wa kwanza wa "Gran Columbia"
  • rais wa kwanza wa Bolivia
  • rais wa pili na wa tatu wa Venezuela
Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Simon Bolivar" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Simon Bolivar kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.