Pangani (mji)

From Wikipedia

Pangani — mji wa kihistoria
Enlarge
Pangani — mji wa kihistoria
Pangani - Boma la Kale
Enlarge
Pangani - Boma la Kale

Mji wa Pangani uko ufukoni mwa Tanzania kati ya Dar es Salaam na Tanga. Leo hii ni mji mdogo mwenye wakazi karibu 8000 na makao makuu ya Wilaya ya Pangani. Lakini ina historia ndefu hasa kwa sababu kuna bandari nzuri ya kiasili mdomoni wa mto wa Pangani inayofaa jahazi ndogo.

Majengo mbalimbali ya kale ni ishara ya historia hiyo. Pamoja na Boma la Wajerumani kuna nyumba za Waswahili.

[edit] Historia

Kuna uwezekano ya kwamba Pangani ina historia ya miaka 2000. Hii inategemea kama kweli Pangani ni sawa na mji wa Rhapta unaojulikana kutokana na kitabu cha Periplus ya Bahari ya Eritrea kilichoandikwa mn. mw. 70 b.K. Walakini siku hizi wataalam wa arkeolojia wanaamini kuwa Rhapta ilikuwepo kwenye sehemu nyingine ya pwani ya Afrika ya Mashariki.

Pangani ilikuwa mji muhimu katika utamaduni wa Waswahili. Katika karne ya 19 BK iliona maendeleo chini ya utawala wa Zanzibar pamoja na miji mingine Uswahilini. Makabaila walilima miwa wakitumia kazi ya watumwa. Pangani ilikuwa pia kituo muhimu ya misafara ilianza hapa kuelekea ndani ya bara pia soko muhimu ya watumwa.

Mwanzo wa ukoloni Pangani ilikuwa mahali pa kuanzishwa kwa vita vya Bushiri mwaka 1889 dhidi ya Wajerumani. Mwakilishi wa Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki (DOAG) von Zelewski alimtendea liwali wa Sultani kwa ukali uliosababisha ghasia ya watu wa Pangani. Baada ya kukomeshwa kwa vita hii umuhimu wa Pangani ulipungua sana kwa sababu Wajerumani walikazia maendeleo ya Tanga. Pia bandari ya Pangani hakufaa tena kupokea meli kubwa.

Polepole Pangani imerudi nyuma. Uhaba wa mawasiliano na barabara uliongeza mwendo huu. Hadi leo hakuna barabara ya lami kabisa katika wilaya yake.

Lugha nyingine