Ottawa

From Wikipedia

Barabara ya Elgin mjini Ottawa
Enlarge
Barabara ya Elgin mjini Ottawa
Majengo ya Bunge ya Kanada
Enlarge
Majengo ya Bunge ya Kanada

Ottawa ni mji mkuu wa Kanada ikiwa ndani ya eneo la jimbo la Ontario. Mji uko kusini ya mto Ottawa. Mwaka 2004 ilikuwa na wakazi 800,000 mjini, pamoja na mitaa ya jirani rundiko la mji lina wakazi 1,146,790 people.

Ottawa ni mji mkubwa wa nne katika Kanada. Wakazi walio wengi hutumia Kiingereza lakini takriban theluji moja ni wasemaji wa Kifaransa kama lugha ya kwanza.

Mto Ottawa wakati wa usiku
Enlarge
Mto Ottawa wakati wa usiku

[edit] Historia

Ottawa iliundwa 1827 ikaitwa mwanzoni Bytown kufuatana na kanali John By aliyesimamia ujenzi wa mfereji kati ya mto Ottawa na mto Rideau na kuanzisha mji vilevile.

Tangu 1857 mji uliteuliwa kama mji mkuu wa koloni ya Amerika ya Kaskazini ya Kiingereza na kuitwa kwa jina la mto Ottawa.

Mahali paliteuliwa kwa sababu ya hofu za vita mpya na Marekani; miji mingine mikubwa ilikuwa karibu mno na mpaka wa Marekani. Faida nyingine ya Ottawa ilikuwa mahali pake kwenye mstari wa mpaka wa ndani kati ya maeneo yanayotumia zaidi lugha ya Kiingereza au lugha ya Kifaransa. Kwa namna hii ilikubaliwa na Wakanada wa kundi zote mbili.

Image:WikiLettreMini.png Makala hiyo kuhusu "Ottawa" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Ottawa kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.