Susenyos
From Wikipedia
Susenyos (takriban 1572 – 7 Septemba, 1632) alikuwa mfalme mkuu wa Uhabeshi kuanzia 1606 hadi muda mfupi kabla ya kifo chake alipojiuzulu. Alimfuata Za Dengel. Jina lake la kutawala lilikuwa Malak Sagad III. Susenyos alivutwa sana na imani ya kikatoliki. Aliwaalika wamisionari na hata kutangaza kuwa Mkatoliki yeye mwenyewe kuanzia mwaka wa 1622. Hata hivyo malodi wengi hawakukubali na utawala ulisumbuliwa na vita na uasi. Mwishoni Susenyos alijiuzulu na kufuatwa na mwana wake, Fasilides aliyerudisha imani ya kiorthodox.
![]() |
Makala hiyo kuhusu "Susenyos" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Susenyos kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |