Maximillian Kolbe
From Wikipedia
Maximilian Kolbe (8 Januari, 1894 – 14 Agosti, 1941) alikuwa padre Mkatoliki katika nchi ya Poland. Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia alifungwa na kuuawa na wafuasi wa Nazi katika kambi ya wafungwa wa siasa kule Auschwitz. Mwaka wa 1982 alitangazwa kuwa mtakatifu. Sikukuu yake ni 14 Agosti.